WANAHABARI WAKONGWE WALIOATHIRIWA NA MFUMO WA ITHIBATI KUREJEA RASMI KWENYE TAALUMA YAO

Date:

Share post:

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda, amesema Serikali imeandaa mwongozo maalumu wa kisheria utakaowawezesha wanahabari wakongwe walioathiriwa na mfumo wa ithibati kurejea rasmi katika taaluma hiyo nchini.

Akisoma hotuba ya wizara hiyo leo Mei 4, 2026, Makonda alisema mwongozo huo umeandaliwa kupitia Bodi ya Uandishi wa Habari Tanzania kwa kuzingatia masharti ya Sheria ya Huduma za Habari, ambayo inalenga kukuza na kuimarisha taaluma ya habari nchini.

Aidha amefafanua kuwa mwongozo huo utaweka utaratibu wa kisheria wa kutambua na kuthibitisha umahiri wa wanahabari hao, hatua itakayowawezesha kupata ithibati ya kitaaluma na kuendelea na shughuli zao kwa mujibu wa sheria.

Hatahivyo Makonda ameongeza kuwa hatua hiyo inalenga kuwapa fursa wanahabari wenye uzoefu mkubwa ambao walijikuta nje ya mfumo rasmi kurejea na kuchangia maendeleo ya sekta ya habari kwa kuzingatia misingi ya taaluma na maadili.

Sanjari na hayo wizara imeeleza kuwa itaendelea kuboresha mifumo na sera mbalimbali ili kuhakikisha taaluma ya habari nchini inakuwa na viwango vinavyokubalika kitaifa na kimataifa.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

KISWAHILI KUIMARISHWA NCHINI KUELEKEA MICHUANO YA AFCON 2027

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda, amesema Serikali imeweka mkazo katika kuimarisha matumizi ya Kiswahili...

‘KARIAKOO DERBY’ YAVUNJA REKODI YA MABAO

BAADA ya sare ya mabao 2-2 jana Mei 3, 2026, mechi inayozikutanisha Simba na Yanga, maarufu kwa jina...

MASTAA WA KIGENI WAENDELEA KUTAMBA ‘KARIAKOO DERBY’

DAKIKA 90 za 'Kariakoo Derby' zilitamatika jana Mei 3, 2026 katika Uwanja wa Jenerali Isamhuyo jijini Dar es...

PANYA, NGUCHIRO WANAVYOTESA RAIA WA PALESTINA UKANDA WA GAZA

JERUSALEM, Palestina NI katika kambi za raia wa Palestina wanaoishi kwenye mahema baada ya makazi yao kusambaratishwa na mashambulizi...