Mkurugenzi wa Jiji la Arusha, Ndugu John Kayombo, amepokea rasmi tuzo maalum pamoja na hundi ya shilingi milioni 8 kwa niaba ya Jiji, kufuatia ushindi wa nafasi ya kwanza kitaifa katika usafi na uhifadhi wa mazingira.
Tuzo hiyo ilitolewa wakati wa maadhimisho ya Wiki ya Afya Kitaifa 2026 yaliyofanyika Wilaya ya Kibiti, Mkoa wa Pwani, ikiwa ni kutambua juhudi kubwa zinazofanywa na Jiji la Arusha katika kuhakikisha mazingira yanakuwa safi na salama kwa afya ya wananchi.






