MADRID YAMPIGA ‘STOP’ ENDRICK

Date:

Share post:

MADRID, Hispania

KLABU ya Real Madrid haina mpango wa kumpiga bei mshambuliaji wake wa kati raia wa Brazil, Endrick, kwa mujibu wa mtandao wa TEAMtalk.

Baada ya kushindwa kung’ara Santiago Bernabeu, Endrick amerejesha makali yake akiwa kwa mkopo Lyon ya Ligue 1.

Akiwa ameshafunga mabao saba na kutoa ‘asisti’ saba katika mechi 18 alizocheza msimu huu, Madrid imepanga kumrejesha na si kumuuza moja kwa moja.

Endrick (19), amekuwa kwenye rada za vigogo wa soka wa Kaskazini mwa Jiji la London, Arsenal na Chelsea.

Katika hatua nyingine, zipo ripoti zinazodai kuwa nyota huyo naye anavutiwa na mpango wa kubaki Madrid na kupigania namba yake kikosini.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

KISWAHILI KUIMARISHWA NCHINI KUELEKEA MICHUANO YA AFCON 2027

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda, amesema Serikali imeweka mkazo katika kuimarisha matumizi ya Kiswahili...

‘KARIAKOO DERBY’ YAVUNJA REKODI YA MABAO

BAADA ya sare ya mabao 2-2 jana Mei 3, 2026, mechi inayozikutanisha Simba na Yanga, maarufu kwa jina...

MASTAA WA KIGENI WAENDELEA KUTAMBA ‘KARIAKOO DERBY’

DAKIKA 90 za 'Kariakoo Derby' zilitamatika jana Mei 3, 2026 katika Uwanja wa Jenerali Isamhuyo jijini Dar es...

PANYA, NGUCHIRO WANAVYOTESA RAIA WA PALESTINA UKANDA WA GAZA

JERUSALEM, Palestina NI katika kambi za raia wa Palestina wanaoishi kwenye mahema baada ya makazi yao kusambaratishwa na mashambulizi...