Monday, June 23, 2025
spot_img

GULAM ATAFAKARI KUPAMBANA NA UBALOZI WA INDIA

Gulam Dewji

 

NA MWANDISHI WETU

MFANYABIASHARI mwenye ukwasi wa kutosha ambaye kampuni, viwanda, mashamba na biashara zake zimetoa ajira kwa Watanzania na raia wa kigeni anatafakari kujibu mapigo dhidi ya Ubalozi wa India uliyoyataja makampuni yake kuwa siyo sehemu salama kufanya kazi.

Wiki iliyopita, siku moja baada ta Gulam kumpa maagizo mmoja wa wasaidizi wake kutuma ujumbe kwa Tanzania PANORAMA Blog wa kusaka suluhu baina ya menejimenti za Kampuni za Mohamedi Enterprises Tanzania Limited (MeTL) na wafanyakazi wa kigeni wanaodai kunyanyaswa alisema anajipanga kujibu mapigo.

Gulam alisema amesikitisha na tamko la ubalozi wa India lililosambazwa mitandaoni kwa sababu linalenga kuwatetea watu wanaomuibia na kumsumbua.

“Ndiyo nimeliona tamko kwani nani kasema hajui kuwa ni tamko la Ubalozi wa India, lakini mimi nasema nakusanya ushahidi halafu nitatoa tangazo kwa vyombo vya habari kwa sababu ubalozi unatetea wezi, unatetea watu wanaoniibia na kunitesa sana na hata polisi wanazo taarifa hizi. Sasa ninazungumza na ubalozi halafu nitatoa statement yangu ambayo mimi nitaitoa kama tangazo,” alisema Gulam.  

AWALI Tanzania PANORAMA Blog, iliripoti kuwa uongozi wa kampuni zilizo chini ya mwamvuli wa Mohamedi Enterprises Tanzania Limited (MeTL) umesema utatafuta njia ya kumaliza mgogoro baina yake na wafanyakazi ambao ni raia wa India katika meza ya mazungumzo.

Hayo yameelezwa na mmoja wa maafisa wa kampuni hiyo aliyetumwa na Mkurugenzi wa MeTL, Gulam Dewji kutoa ufafanuzi kwa Tanzania PANORAMA Blog kuhusu andishi lililowekwa kwenye mitandao ya kijamii likiwatahadhalisha raia wa India wote kuepuka kufanya kazi katika Kampuni za MeTL.

Andiko hilo mtandaoni linaeleza kuwa Ubalozi wa India umekuwa ukipokea kwa mfululizo malalamiko ya wafanyaakazi wa Kampuni za MeTL kunyanyaswa na uongozi pamoja na mwajiri wao kuwafungulia kesi za kughushi mahakamani kiasi cha kusababisha wanafamilia wa wafanyakazi hao kulazimika kurejea India.

Kwamba Mwenyekiti wa Makampuni ya MeTl, Gulam Dewji na maafisa waandamizi wamekuwa wakiwafanyia vitendo vya unyanyasaji na udhalilishaji wafanyakazi hao wanapofikisha malalamiko kwao.

Linahitimishwa kwamba raia wote wa India wasikubali kuajiriwa na Kampuni za MeTL kutokana na mwenendo usiofaa wa viongozi wake wa juu.

Alipoulizwa Mwenyekiti Gulam, kuhusu suala hilo kupitia simu yake ya kiganjani alisema aandikiwe maswali kwa maandishi ili ayajibu na alipoandikiwa, muda mfupi baadaye mtu mmoja mwenye asili ya kiasia alituma ujumbe kwa njia ya whatsapp akieleza kuwa ametumwa na Gulam kufikisha ujumbe kwa Tanzania PANORAMA Blog.

Ujumbe aliuotuma ulisomeka; ‘Bwana Dewji amezungumza na sisi na ametuhakikishia uwajibikaji wa menejimenti katika kulinda maslahi ya wafanyakazi. Tumekubaliana kuwa na mazungumzo ya kina, tungependa kutatua jambo hili kwa njia ya mazungumzo.’

Ujumbe mwingine chini ya huo aliuotuma ulisomeka; ‘leo hii mmelalamika mazingira ya watu wenu ila tusema ukweli pia mnawanyanyasa sana Watanzania sema tu wanashindwa nani wa kuwasemea pia kutokana na hali za maisha yao ila mazingira ya ufanyaji kazi siyo.

Jitahidi za Tanzania PANORAMA Blog kuzungumza na Ubalozi wa India kuhusu suala hili zinaendelea.   

Nyingine Zinazohusiana na Hii

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Tufuatilie

0FansLike
3,913FollowersFollow
0SubscribersSubscribe
- Advertisement -spot_img

Habari Nyingine Mpya