‘WASAUZI’ WAINGILIA DILI LA NWABALI KUTUA SIMBA

Date:

Share post:

Na mwandishi wetu

MPANGO wa Simba kumsajili kipa wa timu ya Taifa ya Nigeria ‘Super Eagles’, Stanley Nwabali, umeifikia Kaizer Chiefs na sasa klabu hiyo ya Afrika Kusini nayo inamtolea macho.

Nwabali amekuwa mchezaji asiye na klabu tangu alipoachana na Chippa United aliyojiunga nayo mwaka 2022 akitokea Katsina United.

Alionesha kiwango bora wakati wa fainali za AFCON 2025 na kuzivutia klabu kadhaa kubwa, zikiwamo Al Ettifaq ya Saudi Arabia na QPR ya Ligi Daraja la Kwanza ya England (Championship).

Kwa wiki za hivi karibuni, mlinda mlango huyo amekuwa akihusishwa na soka la Tanzania, akitajwa kuwa kwenye rada za Simba.

Hata hivyo, sasa Wekundu wa Msimbazi watalazimika kuongeza kasi kwani mabosi wa Kaizer Chiefs nao wanamtolea macho nyota huyo wa zamani wa Enyimba.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

RAIS WA TAIWAN ASITISHA ZIARA YAKE AFRIKA, CHINA IKITAJWA KUWA CHANZO

TAIPEI, TaiwanRAIS wa Taiwan, Lai Ching-te, ameahirisha ziara yake nchini Eswatini, huku akiitaja China kuwa ndiyo chanzo cha...

USIYOYAJUA KUHUSU ZIARA YA PAPA LEO BARANI AFRIKA

KIONGOZI wa Kanisa Katoliki duniani, Papa Leo XIV, yuko barani Afrika kwa ziara ya siku 10 katika mataifa...

MATESO WANAYOPITIA WATOTO KATIKA MACHAFUKO YA SUDAN

DARFUR, Sudan "HALI ya watoto nchini Sudan inazidi kuwa mbaya kila baada ya saa moja." Hiyo ni kauli ya...

IRAN: TUKO TAYARI KWA VITA MAZUNGUMZO YAKISHINDIKANA

TEHRAN, IranSPIKA wa Bunge la Iran, Mohammad Bagher Ghalibaf, amesema nchi yake itakuwa tayari kwa mbinu mpya za...