SERIKALI YAINGILIA KATI UCHAGUZI WA TOC

Date:

Share post:

Serikali kupitia Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda, imesitisha uchaguzi wa Kamati ya Olimpiki Tanzania (TOC) uliokuwa ufanyike Aprili 12, 2026.

Uamuzi huo umechukuliwa kufuatia malalamiko yaliyotolewa na baadhi ya wagombea, wakidai kukosekana kwa uwazi, haki na usawa katika mchakato mzima wa uchaguzi huo.

Akizungumza kuhusu hatua hiyo, Serikali imeeleza kuwa kusitishwa kwa uchaguzi ni hatua ya muda inayolenga kutoa nafasi kwa uchunguzi huru kufanyika pamoja na kurekebisha kasoro zilizojitokeza katika mchakato huo.

Aidha, imeelezwa kuwa kamati ya muda imeundwa kusimamia shughuli za TOC wakati uchunguzi ukiendelea. Kamati hiyo itashirikiana na taasisi mbalimbali ikiwemo TAKUKURU na Jeshi la Polisi ili kuhakikisha haki inatendeka na taratibu zote zinafuatwa ipasavyo.

Serikali imesisitiza dhamira yake ya kuhakikisha uchaguzi wa haki na uwazi unafanyika mara baada ya uchunguzi kukamilika.

About The Author

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

USIYOYAJUA KUHUSU KOCHA ALIYEANDIKA HISTORIA BUNDESLIGA

MUNICH, Ujerumani JINA la Marie-Louise Eta limeandika historia katika soka la Ujerumani baada ya kuwa mwanamke wa kwanza kuwa...

BURNA BOY HATAKI MAZOEA, ‘BIFU’ KWAKE KAWAIDA TU

HIVI karibuni, supastaa wa muziki wa Afrobeat, Burna Boy, aliingia kwenye mikono ya Chama cha 'Ma-dj' nchini Nigeria,...

BURKINA FASO IKO HOI AU HAI CHINI YA KAPTENI TRAORE?

HATUA ya kutangaza kuwa raia wake waaitarajie demokrasia imeibua maswali mengi juu ya uongozi wa Kapteni Ibrahim Traore...

SIMU YAKO CHANZO CHA UGONJWA WA MOYO, SARATANI?

UKWELI ulio wazi ni kwamba matumizi ya simu za mkononi yameongezeka kwa kasi duniani, Tanzania ikiwa na 'laini'...