RAIS WA CUBA AIVIMBIA MAREKANI, AGOMA KUJIUZULU

Date:

Share post:

HAVANA, Cuba

RAIS wa Cuba, Miguel Diaz-Canel, amesema hatojiuzulu kwa sababu ya shinikizo la Serikali ya Marekani.

Ikumbukwe kuwa kwa muda mrefu sasa, uhusiano wa Marekani na Cuba umekuwa wa kutilia shaka na wakati fulani Rais Donald Trump alitishia kuivamia kijeshi.

Diaz-Canel amesema hatishwi na presha anayopewa na Marekani. “Kujiuzulu siyo sehemu ya misamiati yetu,” amesema.

Akihojiwa na Shirika la Utangazaji la NBC, amesema Cuba ni nchi huru na inayopaswa kuheshimiwa katika uendeshaji wa mambo yake.
Ameongeza kuwa Kisiwa hicho hakipaswi kuwa koloni la Marekani kwa kusikiliza na kupokea maagizo kutoka kwa Taifa hilo.

“Kwa hapa Cuba, viongozi wanaoingia madarakani huwa hawachaguliwi na Serikali ya Marekani,” amesema.

Imeandaliwa na Hassan Mwasha

About The Author

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

USIYOYAJUA KUHUSU KOCHA ALIYEANDIKA HISTORIA BUNDESLIGA

MUNICH, Ujerumani JINA la Marie-Louise Eta limeandika historia katika soka la Ujerumani baada ya kuwa mwanamke wa kwanza kuwa...

BURNA BOY HATAKI MAZOEA, ‘BIFU’ KWAKE KAWAIDA TU

HIVI karibuni, supastaa wa muziki wa Afrobeat, Burna Boy, aliingia kwenye mikono ya Chama cha 'Ma-dj' nchini Nigeria,...

BURKINA FASO IKO HOI AU HAI CHINI YA KAPTENI TRAORE?

HATUA ya kutangaza kuwa raia wake waaitarajie demokrasia imeibua maswali mengi juu ya uongozi wa Kapteni Ibrahim Traore...

SIMU YAKO CHANZO CHA UGONJWA WA MOYO, SARATANI?

UKWELI ulio wazi ni kwamba matumizi ya simu za mkononi yameongezeka kwa kasi duniani, Tanzania ikiwa na 'laini'...