CMT YAFANYA ZIARA YA KUTEMBELEA MIRADI YA MAENDELEO KOROGWE

Date:

Share post:

Timu ya Menejimenti ya Halmashauri ya Mji Korogwe (CMT) imefanya ziara ya kutembelea na kukagua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa katika maeneo tofauti ya halmashauri ya korogwe.

Ziara hiyo imeongozwa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Korogwe Bi. Zahara Msangi akishirikiana na wakuu wa idara na vitengo, ikiwa na lengo la kufuatilia maendeleo ya miradi, kuhakikisha thamani ya fedha inaonekana pamoja na kubaini changamoto zinazojitokeza katika utekelezaji wake.Katika ziara hiyo, CMT ilitembelea miradi ya sekta mbalimbali ikiwemo elimu na mradi wa maendeleo wa vijana wa mji huo.

Akizungumza katika ziara hiyo, Bi. Zahara Msangi ametoa wito kwa wasimamizi wa miradi kuhakikisha miradi hiyo inakamilika kwa ubora unaotakiwa huku akitoa angalizo kwa wasimamizi hao kusimamia miradi hiyo kwa uweledi ilikuepusha kuisababishia serikali hasara.

Ziara za aina hii zinasaidia kuongeza ufanisi katika usimamizi wa miradi ya maendeleo pamoja na kuhakikisha huduma bora zinawafikia wananchi kwa wakati

About The Author

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

USIYOYAJUA KUHUSU KOCHA ALIYEANDIKA HISTORIA BUNDESLIGA

MUNICH, Ujerumani JINA la Marie-Louise Eta limeandika historia katika soka la Ujerumani baada ya kuwa mwanamke wa kwanza kuwa...

BURNA BOY HATAKI MAZOEA, ‘BIFU’ KWAKE KAWAIDA TU

HIVI karibuni, supastaa wa muziki wa Afrobeat, Burna Boy, aliingia kwenye mikono ya Chama cha 'Ma-dj' nchini Nigeria,...

BURKINA FASO IKO HOI AU HAI CHINI YA KAPTENI TRAORE?

HATUA ya kutangaza kuwa raia wake waaitarajie demokrasia imeibua maswali mengi juu ya uongozi wa Kapteni Ibrahim Traore...

SIMU YAKO CHANZO CHA UGONJWA WA MOYO, SARATANI?

UKWELI ulio wazi ni kwamba matumizi ya simu za mkononi yameongezeka kwa kasi duniani, Tanzania ikiwa na 'laini'...