WASHINGTON DC, Marekani
MKE wa Rais Donald Trump, Melania Trump, amesema hajawahi kuwa na uhusiano na Jeffrey Epstein, hivyo hataki tena kusikia stori hizo.
Melania ameyasema hayo katika mkutano wake na waandishi wa habari uliofanyika Ikulu.
Epstein aliyekwishafariki, alikuwa na tuhuma nyingi za udhalilishaji wa kingono, ikisemekana kuwa ndiye aliyewakutanisha Melania na Trump.
Hata hivyo, Melania amekanusha uvumi huo akiuita kuwa ni jitihada za kuharibu heshima na jina lake.
Licha ya kukiri kufahamiana na Epstein, Melania amesema: “Sikuwahi kufahamu chochote kuhusu Epstein kujihusisha na tabia hizo. Sihusiki.”






