MANCHESTER, Uingereza
KLABU ya Manchester United inampigia hesabu kali kiungo wa Southampton, Shea Charles.
Nyota huyo mwenye umri wa miaka 22, ndiye aliyefunga bao la ushindi wakati Southampton ilipoifunga Arsenal mabao 2-1 katika mchezo wa hivi karibuni wa robo fainali ya Kombe la FA.
Charles alitua Southampton mwaka 2023 akitokea Manchester City na ameshacheza mechi 67, akifunga mabao manne na ‘asisti’ mbili.
Kiwango chake bora kimezivutia klabu kadhaa, zikiwamo pia Everton na Nottingham Forest, huku thamani yake sokoni ikiwa ni Pauni milioni 20.
Man United inamtolea macho wakati huu ikiwa inajiandaa kumpiga bei Manuel Ugarte, huku kiungo mwingine, Casemiro, naye akiwa njiani kuondoka.






