ATLETICO MADRID YAVUNJA MWIKO CAMP NOU

Date:

Share post:

CATALUNYA, Hispania

KWA ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Barcelona, Atletico Madrid ya kocha Diego Simeone imefuta ‘mkosi’ ulioiandama kwa miaka 20.

Katika mchezo wa jana Aprili 8, 2026 wa robo fainali ya kwanza ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, Atletico ikiwa ugenini ilipata mabao yake kupitia Julian Alvarez na Alexander Sorloth.

Rekodi zinaonesha kuwa ushindi huo ni wa kwanza kwa Atletico ikiwa Camp Nou tangu mwaka 2006.

Atletico iliposhinda ugenini mabao 2-1 dhidi ya Barcelona mwaka 2024, mechi hiyo ilichezwa katika Uwanja wa Estadi Olimpic Lluis Companys.

Ni dimba walilokuwa wakitumia Barcelona kwa dharura wakati Camp Nou ikiwa kwenye maboresho.

Katika Uwanja wa Camp Nou, Atletico imepoteza mech zote 25 ilizocheza hapo tangu mwaka 2006.

About The Author

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

USIYOYAJUA KUHUSU KOCHA ALIYEANDIKA HISTORIA BUNDESLIGA

MUNICH, Ujerumani JINA la Marie-Louise Eta limeandika historia katika soka la Ujerumani baada ya kuwa mwanamke wa kwanza kuwa...

BURNA BOY HATAKI MAZOEA, ‘BIFU’ KWAKE KAWAIDA TU

HIVI karibuni, supastaa wa muziki wa Afrobeat, Burna Boy, aliingia kwenye mikono ya Chama cha 'Ma-dj' nchini Nigeria,...

BURKINA FASO IKO HOI AU HAI CHINI YA KAPTENI TRAORE?

HATUA ya kutangaza kuwa raia wake waaitarajie demokrasia imeibua maswali mengi juu ya uongozi wa Kapteni Ibrahim Traore...

SIMU YAKO CHANZO CHA UGONJWA WA MOYO, SARATANI?

UKWELI ulio wazi ni kwamba matumizi ya simu za mkononi yameongezeka kwa kasi duniani, Tanzania ikiwa na 'laini'...