CATALUNYA, Hispania
KWA ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Barcelona, Atletico Madrid ya kocha Diego Simeone imefuta ‘mkosi’ ulioiandama kwa miaka 20.
Katika mchezo wa jana Aprili 8, 2026 wa robo fainali ya kwanza ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, Atletico ikiwa ugenini ilipata mabao yake kupitia Julian Alvarez na Alexander Sorloth.
Rekodi zinaonesha kuwa ushindi huo ni wa kwanza kwa Atletico ikiwa Camp Nou tangu mwaka 2006.
Atletico iliposhinda ugenini mabao 2-1 dhidi ya Barcelona mwaka 2024, mechi hiyo ilichezwa katika Uwanja wa Estadi Olimpic Lluis Companys.
Ni dimba walilokuwa wakitumia Barcelona kwa dharura wakati Camp Nou ikiwa kwenye maboresho.
Katika Uwanja wa Camp Nou, Atletico imepoteza mech zote 25 ilizocheza hapo tangu mwaka 2006.






