LONDON, Uingereza
WINGA wa Chelsea, Alejandro Garnacho, ameingia kwenye rada za klabu kongwe ya Argentina, River Plate.
Ni mwaka mmoja sasa tangu Muargentina huyo mwenye umri wa miaka 21 alipojiunga na Chelsea akitokea Manchester United.
Garnacho aliondoka Old Trafford baada ya kumkosoa hadharani kocha wa wakati huo, Ruben Amorim.
Hata hivyo, mambo hayajaenda vizuri kwake chini ya kocha mpya wa Blues, Liam Rosenior.
Wakati huu akiwa hana furaha, ripoti zinaeleza kuwa kocha wa Plate, Eduardo Coudet, amefanya mawasiliano ya moja kwa moja na winga huyo.







