JELA MIAKA 15 KWA KUSABABISHA KIFO CHA MWIGIZAJI

Date:

Share post:

LOS ANGELES, Marekani

MWANAMKE aliyejulikana kwa jina la Jasveen Sangha amehukumiwa kifungo cha miaka 15 gerezani baada ya dawa alizompatia Matthew Perry kusababisha kifo cha mwigizaji huyo.

Perry ni staa wa soko la filamu nchini  gMarekani (Hollywood) na moja ya kazi zake maarufu ni ‘Friends’.

Alikutwa amefariki nyumbani kwake mjini Los Angeles mwishoni mwa mwaka 2023 na uchunguzi kubaini kuwa alizidiwa na dawa hizo.

Jasveen mwenye umri wa miaka 42, maarufu pia kwa jina la ‘Ketamine Queen’, alikutwa na hatia Septemba, 2025.

Ni baada ya kubainika kuwa alimpatia Perry dawa aina ya ketamine, ambazo mbali ya matumizi mengine, husaidia kupunguza maumivu.

Waendesha Mashitaka wameeleza kuwa nyumba ya bibiye huyo ni ghala la kuhifadhi dawa hizo na amekuwa akiwauzia watu wengi maarufu.

About The Author

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

USIYOYAJUA KUHUSU KOCHA ALIYEANDIKA HISTORIA BUNDESLIGA

MUNICH, Ujerumani JINA la Marie-Louise Eta limeandika historia katika soka la Ujerumani baada ya kuwa mwanamke wa kwanza kuwa...

BURNA BOY HATAKI MAZOEA, ‘BIFU’ KWAKE KAWAIDA TU

HIVI karibuni, supastaa wa muziki wa Afrobeat, Burna Boy, aliingia kwenye mikono ya Chama cha 'Ma-dj' nchini Nigeria,...

BURKINA FASO IKO HOI AU HAI CHINI YA KAPTENI TRAORE?

HATUA ya kutangaza kuwa raia wake waaitarajie demokrasia imeibua maswali mengi juu ya uongozi wa Kapteni Ibrahim Traore...

SIMU YAKO CHANZO CHA UGONJWA WA MOYO, SARATANI?

UKWELI ulio wazi ni kwamba matumizi ya simu za mkononi yameongezeka kwa kasi duniani, Tanzania ikiwa na 'laini'...