WASHINGTON DC, Marekani
RAIS wa Marekani, Donald Trump, amelijia juu Shirika la Utangazaji la CNN akisema limekuwa likizalisha habari za uongo.
Trump hajafurahishwa na namna CNN ilivyoripoti kuwa makubaliano ya Marekani na Iran kusitisha vita kwa wiki mbili ni ushindi kwa Taifa hilo la Kiarabu.
Katika taarifa yake, CNN ilieleza kuwa Iran imeipa masharti kadhaa Marekani na yalipokubaliwa, ndipo ilipoafiki suala ya kusimamisha vita.
Lakini, jambo hilo limepingwa vikali na Trump akisema CNN wamepata taarifa hiyo ya uongo kutoka katika tovuti moja nchini Nigeria.
Hata hivyo, CNN wamekanusha kile alichokisema Trump, kwamba taarifa hiyo imetoka Nigeria, wakisisita kuwa walifanya mahojiano na viongozi wa Iran.
Aidha, amesema mamlaka zinapima athari za taarifa hiyo ya CNN na kama imekiuka sheria, basi hatua zaidi zitachukuliwa, ikiwamo kufunguliwa mashitaka.






