KLABU ya Coastal Union, imetangaza kuachana na kocha wake mkuu, Mohammed Muya, kufuatia mwenendo usioridhisha wa timu hiyo katika mashindano ya Ligi Kuu Tanzania Bara.
Kupitia ukurasa wao wa kijamii, uongozi wa klabu hiyo umeeleza kuwa umefikia makubaliano ya pande zote kusitisha kandarasi na kocha huyo.
Aidha, klabu hiyo imesema itatangaza hivi karibuni muundo mpya wa benchi la ufundi.
Kwa sasa, Coastal Union, maarufu kama Wagosi wa Kaya, wanashika nafasi ya 13 kwenye msimamo wa ligi wakiwa na alama 16 baada ya kucheza mechi 18.






