Washington, Marekani
Rais wa Marekani Donald J Trump amesema kuwa akimaliza awamu yake ya uongozi nchini humo, anaweza kwenda kugombea urais nchini Venezuela na akapata kura nyingi kuliko mtu mwingine yeyote katika historia ya nchi hiyo.
“watu wa Venezuela wanasema kama nitagombea urais wa Venezuela, nitapata kura nyingi kuliko alizowahi kupata mtu mwingine yeyote, kwahiyo nikimaliza hili ninaweza kwenda Venezuela, nikajifunza kihispania kwa rahara, haitachukua muda mrefu kwasababu mimi ni mzuri kwenye lugha…….lakini tunafuraha na rais aliyechaguliwa”
Kauli hii ya Trump inakuja ikiwa imepita takribani miezi mitatu tangu aliyekuwa Rais wa Venezuela Nicolás Maduro,avamiwe na kukamatwa akiwa nchini kwake kisha kupelekwa nchini Marekani na kufunguliwa mashitaka.






