RIPORA PANORAMA
SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar imesema kuwa licha ya vita vinavyoendelea katika baadhi ya nchi za Mashariki ya Kati ambazo ni wazalishaji wakubwa wa mafuta duniani, Zanzibar ina akiba ya kutosha ya nishati hiyo na hakuna dalili ya upungufu kwa sasa.
Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Maji, Nishati na Madini, Nadil Abdul-latif wakati akizungumza na waandishi wa habari akitoa tathmini ya mafanikio ya siku 100 za uongozi wa Rais wa Zanzibar, Dk. Hussein Ali Mwinyi katika kipindi chake cha pili.
Amesema hatua zilizochukuliwa na serikali kukabiliana na athari za kiuchumi na kibiashara zinazoweza kujitokeza kutokana na migogoro hiyo ya kimataifa.
Waziri huyo, amesema serikali imejipanga kuhakikisha upatikanaji wa mafuta unaendelea kuwa wa uhakika visiwani humo bila changamoto yoyote kwa wananchi na sekta mbalimbali za uzalishaji.
