RIPOTA PANORAMA
MTANDAO wa Polisi Wanawake (TPF NeT) Wilaya ya Rungwe, Mkoa wa Mbeya umewataka Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Bulyaga kushiriki kutokomeza ukatili katika jamii.
Rai hiyo imetolewa na Mkaguzi wa Polisi, Fausta Ndumbaro walipotembelea shule hiyo Machi 04, 2026 na kutoa elimu ya kupinga vitendo vya ukatili na unyanyasaji dhidi ya watoto.
Mkaguzi wa Polisi Ndumbaro amewataka wanafunzi hao kushirikiana na Jeshi la Polisi na taasisi nyingine katika vita ya kuzuia na kutokomeza vitendo vya ukatili na unyanyasaji dhidi ya watoto kwa kutoa taarifa na kuwafichua wanaofanya vitendo hivyo.

Naye, Polisi Kata ya Kinyala, Mkaguzi wa Polisi, Lusajo Kibonde amewakumbusha wanafunzi hao wajibu wao kama watoto katika familia ikiwemo utoaji wa taarifa za viashiria vya uhalifu, kusaidia wazazi/walezi kazi za nyumbani na kusoma kwa bidii.

Katika kuelekea maadhimisho ya siku ya mwanamke duniani, Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya lipo katika muendelezo wa utoaji elimu ya kijinsia na ukatili kwa makundi mbalimbali ya kijamii ili kuyajengea uwezo na uelewa wa masuala hayo.
