MWANDISHI WETU
ZANZIBAR:
MSEMAO wa ‘mtani hutoki leo’ umekuwa maarufu nje ya Uwanja wa Amani, Visiwani Zanzibar ambapo mashabiki mbalimbali wa Yanga na Simba wamekuwa wakitumia msemo huo kila walipotambiana kabla ya mechi yao itakayopigwa usiku wa saa 2:30 katika dimba la Aman Complex.
Mashabiki hawa wametoka ndani ya Zanzibar nikimaanisha Unguja na Pemba na wapo waliotoka mikoa mbalimabli ya Bara.
Mechi hii iliyovuta sura ya ‘vita ya heshima au ubabe’ ambapo kama Simba atafungwa mara ya saba Yanga wataonekana wababe na kama Simba atashinda itakuwa ni heshima.

Derby hiyo haiishia katika utani wa jadi nje ya uwanja bali imeleta manufaa kwa wauzaji wa vitu mbalimbali vinavyohusika na mchezo huo vikiwemo jezi, vikombe, vuvuzela, kofia, bendera na skafu.
Je, Simba atavunja mwiko wa kupigwa ama Yanga atabaki kuwa mbabe kwa mara ya saba?
