DAR ES SALAAM
TUME ya uchunguzi wa matukio ya uvunjifu wa amani yaliyotokea wakati na baada ya uchaguzi mkuu wa Oktoba 29, 2025, Februari 27, 2026 ilikutana na kiongozi mkuu wa masuala ya sheria ya kiislamu na uongozi wa waislamu Tanzania, Mufti Sheikh Abubakar Zubeir.
Mkutano huo wa Tume na Mufti ulifanyika katika Ukumbi wa Lake Tanganyika uliopo Jengo la Benki Kuu ya Tanzania (BoT) jjini hapa.
Miongoni mwa yaliyojadiliwa ni pamoja na namna matukio hayo yalivyoanza, athari zake kwa watu, mali na miundombinu pia ushauri wa namna ya kuondokana na matukio hayo.
Hivi karibuni, mamlaka ya uteuzi iliiongezea tume muda wa siku arobaini na mbili (42) kuanzia Februari 20, 2026 ili iweze kukamilisha uchunguzi wa matukio hayo.
Tume inatakiwa kukamilisha kazi na kuwasilisha taarifa yake kabla au Aprili 3, 2026.
