KARDINALI PENGO AFARIKI DUNIA

Date:

Share post:

RIPOTA PANORAMA

ALIYEKUWA Askofu Mkuu Mstaafu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Polycarp Kardinal Pengo, amefariki dunia Februari 19, 2026 majira ya saa nne usiku.

Taarifa za kifo chake ilitolewa jana usuki na Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Thaddeus Ruwa’ichi kwa waraka wa kanisa uliotumwa kwa makardinali, maaskofu, mapadre, watawa na waumini wote wa kanisa hilo.

Katika waraka huo, Askofu Mkuu Ruwa’ichi amesema Kardinali Pengo alifariki akiwa kwenye matibabu katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) jijini Dar es Salaam.

“Ninayo masikitiko makubwa kuwatangazieni kwamba mpendwa baba yetu Mwadhama Polycarp Kardinal Pengo, Askofu Mkuu Mstaafu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, ameitwa nyumbani kwa Baba wa Milele akiwa katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) jijini Dar es Salaam,” ameeleza Ruwa’ichi

Kuhusu mipango ya mazishi amesema taarifa zitatolewa baadaye baada ya maandalizi kukamilika, huku waamini wakihimizwa kuendelea kumuombea marehemu apumzike kwa amani.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

SOMA HIYO! ISRAEL NDIYO WAASISI WA MIKWAJU YA PENALTI

LONDON, Uingereza NI jioni ya Agosti 5, 1970 kwenye Uwanja wa Boothferry Park mjini Hull, Manchester United ikiwa ugenini...

AMEJIPATA! LAMPARD ALIVYOREJEA EPL AKIWEKA REKODI

LONDON, Uingereza IKIWA ni miezi 18 tu imepita tangu alipoajiriwa, Frank Lampard ameiwezesha Coventry City kupanda daraja na kurejea...

USICHUKULIE POA! PATORANKING ALIUZA SUMU YA PANYA MITAANI KABLA YA ‘KUTOBOA’

LAGOS, Nigeria WAHENGA walisema maisha ni safari yenye milima na mabonde. Kwamba katika kuishi kwako, si nyakati zote zitakuwa...

KIFO CHA BOSI KINAVYOITESA LEICESTER CITY

LONDON, UingerezaMIAKA 10 iliyopita, Leicester City waliishangaza dunia walipotwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya England (EPL) mbele ya...