KIJAJI ATAKA TANAPA KUZINGATIA UTU

Date:

Share post:

RIPOTA PANORAMA

WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Dk. Ashatu Kijaji amewataka wafanyakazi wa Shirika la Hifadhi za Taifa, (TANAPA) kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia utu ili kuboresha ustawi wa jamii.

Akizungumza na wafanyakazi wa shirika hilo makao makuu ya TANAPA hivi karibuni, Waziri Kijaji aliwataka kuzingatia kauli mbiu ya Rais Samia Suluhu Hassan ya kazi na utu wanapotekeleza majukumau yao ya uhifadhi.

Alisisitiza kuwa wafanyakazi wa shirika hilo wanapaswa kuwa wabunifu kutangaza vivutio vya utalii ili serikali iweze kufikia lengo lake la kuongeza watalii wanaotembeela Hifadhi za Taifa hadi kufikia milioni nane ifikapo 2030.

Akimkaribisha kuzungumza na watumishi hao, Kamishna wa Uhifadhi wa TANAPA, Mussa Nassoro Kuji alitoa taarifa ya maendeleo ya miundombinu na ongezeko la watalii na mapato yatokanayo na utalii.

Kamishna Kuji alisema kipindi cha robo ya kwanza ya mwaka wa fedha 2025/26 Hifadhi za Taifa zilitembelewa na watalii 62,468 ikiwa ni zaidi ya lengo la watalii 61,742 na kwa wastani ni ongezeko la asilimia 1.18.

“Kwa idadi hiyo, mapato yaliyokusanywa ni shilingi bilioni 3.9 sawa na ongezako la asilimia 15.44,” alisema Kamishna Kuji.

   

About The Author

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

USIYOYAJUA KUHUSU KOCHA ALIYEANDIKA HISTORIA BUNDESLIGA

MUNICH, Ujerumani JINA la Marie-Louise Eta limeandika historia katika soka la Ujerumani baada ya kuwa mwanamke wa kwanza kuwa...

BURNA BOY HATAKI MAZOEA, ‘BIFU’ KWAKE KAWAIDA TU

HIVI karibuni, supastaa wa muziki wa Afrobeat, Burna Boy, aliingia kwenye mikono ya Chama cha 'Ma-dj' nchini Nigeria,...

BURKINA FASO IKO HOI AU HAI CHINI YA KAPTENI TRAORE?

HATUA ya kutangaza kuwa raia wake waaitarajie demokrasia imeibua maswali mengi juu ya uongozi wa Kapteni Ibrahim Traore...

SIMU YAKO CHANZO CHA UGONJWA WA MOYO, SARATANI?

UKWELI ulio wazi ni kwamba matumizi ya simu za mkononi yameongezeka kwa kasi duniani, Tanzania ikiwa na 'laini'...