MAJALIWA AFARIJIKA NA SENSA YA KIDIJITALI

Date:

Share post:

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa


RIPOTA WA WAZIRI MKUU

WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema amefarijika jinsi shughuli ya sensa ya watu na makazi ilivyoanza mwaka huu na kupokelewa katika maeneo mbalimbali nchini.

Kauli hiyo ameitoa leo mchana baada ya kumaliza kuhojiwa na karani wa sensa nyumbani kwake, Kijiji cha Namahema, Kata ya Nandagala, Wilaya ya Ruangwa, mkoani Lindi.

“Kwa kweli nina faraja sana kwamba kati ya sensa zilizofanyika hapa nchini, hii ya mwaka huu Watanzanua wameipokea vizuri na wamehamasika sana,” amesema.

Amewashukuru viongozi wakuu wa kitaifa, Rais Samia Suluhu Hassan, Makamu wa Rais, Dk. Philip Mpango na Rais wa Zanzibar, Dk. Hussein Ali Mwinyi kwa hamasa walizotoa wakati wa kuhamasisha umma.

“Pia ninawashukuru sana viongozi wa dini kwa kutoa hamasa kupitia nyumba za ibada na kipekee zaidi vyombo vya habari ambavyo vimefanya kazi kubwa ya kuhamasisha wananchi,” amesema.

Amesema sensa ya mwaka huu ni ya aina yake kwa sababu inajumuisha uratibu wa mfumo wa anuani za makazi ambao haukuwepo kwenye sensa tano zilizotangulia na pia inaenda kwa mifumo ya kidigitali ambapo mifumo ya teknolojia ya habari na mawasiliano (TEHEMA) inatumika.

“Awamu tano zilizopita huyu karani hapa angekuwa na makaratasi mengi ya madodoso kibao lakini kutokana na mfumo huo ana kifaa kimoja tu ambacho kimebeba maswali yote. Mimi hapa nimejibu maswali 100 ndani ya muda mfupi kwa kutumia kifaa hicho,” amesema.

Amewataka wananchi ambao hawajafikiwa wasiwe na hofu kwani sensa hii ina maswali madogomadogo ambayo hayalengi kuleta tafrani bali yenye kulenga kupata taarifa za kuisaidia nchi kupanga mipango ya kuleta maendeleo.

 

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

SOMA HIYO! ISRAEL NDIYO WAASISI WA MIKWAJU YA PENALTI

LONDON, Uingereza NI jioni ya Agosti 5, 1970 kwenye Uwanja wa Boothferry Park mjini Hull, Manchester United ikiwa ugenini...

AMEJIPATA! LAMPARD ALIVYOREJEA EPL AKIWEKA REKODI

LONDON, Uingereza IKIWA ni miezi 18 tu imepita tangu alipoajiriwa, Frank Lampard ameiwezesha Coventry City kupanda daraja na kurejea...

USICHUKULIE POA! PATORANKING ALIUZA SUMU YA PANYA MITAANI KABLA YA ‘KUTOBOA’

LAGOS, Nigeria WAHENGA walisema maisha ni safari yenye milima na mabonde. Kwamba katika kuishi kwako, si nyakati zote zitakuwa...

KIFO CHA BOSI KINAVYOITESA LEICESTER CITY

LONDON, UingerezaMIAKA 10 iliyopita, Leicester City waliishangaza dunia walipotwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya England (EPL) mbele ya...