KIKOSI CHA KUOGELEA CHATAJWA HADHARANI

Date:

Share post:

KIKOSI cha Tanzania cha Kuogelea kimetajwa hadharani kwa ajili ya kujiandaa na michuano ya ‘Africa Acquatics’, Kanda ya 3, iliyopangwa kufanyika Oktoba 16-19, mwaka huu.

Akizungumza na Panorama, Mkurugenzi wa Ufundi wa Chama cha Kuogelea Tanzania (TSA), Amina Mfaume, alisema wametangaza kikosi cha awali wakiwamo waogeleaji chipukizi na wakongwe kwa ajili ya kujiandaa na michuano hiyo.

Amina alisema katika kikosi hicho wameitwa waogeleaji wenye umri wa kuanzia miaka 17 kwa lengo la kupata kikosi bora endelevu cha Taifa.

Alisema timu ya ufundi ya TSA, imepanga waogeleaji wataanza mazoezi Agosti mwaka huu, chini ya makocha wa Taifa, wakiongozwa na kocha mkuu Alexander Mwaipasa.

Makocha wengine watakaokinoa kikosi hicho ni pamoja na Agnes Kimimba, Kanisi Mabena na Ally Msaizi.

About The Author

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

UCHUMI WA CHINA WAZIDI KUIMARIKA

BEIJING, China LICHA ya vita vya Marekani na Iran kuonekana kuitikisa dunia, China imeendelea kupiga hatua kubwa katika eneo...

SIKU 100 ZA RAIS MPYA WA VENEZUELA: MABADILIKO NA MASWALI MAPYA

CARACAS, Venezuela BAADA ya vikosi vya Marekani kumng’oa madarakani aliyekuwa Rais wa Venezuela, Nicolás Maduro kwenye oparesheni ya Januari...

MAELFU YA FAMILIA SUDAN BADO WAKIMBIA VITA, HALI YA MAISHA YAZIDI KUWA MBAYA

MAELFU ya familia nchini Sudan bado wanalazimika kuyakimbia makazi yao, miji na hata mipaka ya nchi kufuatia vita...

ISRAEL YAENDELEA NA OPERESHEN DHIDI YA HEZBOLLAH NCHINI LEBANON

Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu amesema Jeshi la nchi yake linaendelea na operesheni dhidi ya wanamgambo wanaoungwa...