KANYANI AANZA KUJIBU TUHUMA ANAZOELEKEZEWA

Date:

Share post:

Salim Kanyani

 

RIPOTA PANORAMA

0711 46 49 84

SALIM Kanyani anayetajwa kuwa mganga wa kienyeji aliyejipatia fedha nyingi kwa njia ya ulaghai ameanza kujibu tuhuma anazoelekezewa.

Kanyani ameiambia Tanzania PANORAMA Blog hivi karibuni kwa njia ya simu kuwa yeye siyo mganga wa kienyeji kama inavyodaiwa na mfanyabiashara Remoy Kibombe, bali alikuwa akimsaidia kufuata dawa za kienyeji kwa waganga sehemu mbalimbali za mikoa ya kanda ya ziwa.

Amesema, mbali na kumsaidia kufuata dawa kwa waganga wa kienyeji pia alimuokoa kutoka kwenye mikono ya matapeli waliokuwa wakila hela zake kwa kumdanganya kuwa watamtafutia dawa za matatizo yake.

“Mimi sipo Dar es Salaam lakini nitakuja kuwaeleza vizuri kuhusu hilo suala. Mwanzo sikuweza kuongea na nyie vizuri kwa sababu sikuamini kuwa ninyi ni waandishi wa habari kweli lakini baada ya kusoma taarifa zenu nimeamini na nawaahidi nitakuja kuzungumza na nyie mjue ukweli.

“Kwa sasa ninachoweza kusema ni kwamba mimi siyo mganga wa kienyeji ila ninawafahamu waganga wengi. Kibombe nilikuwa namsaidia kufuata dawa kwa waganga wa kienyeji sehemu mbalimbali za mikoa ya kanda ya ziwa.

“Nadhani unajua kuwa dawa za kienyeji hazina bei rasmi, ni maelewano hivyo mimi nilikuwa nampa bei waliyokuwa wanasema hao waganga kama ni milioni sita au kumi ananipa namfuata dawa na hilo sidhani kama ni kosa.

“Huyo Kibombe nilimkuta anaendeshwa vibaya na wajanja fulani ambao walikuwa wanamlia hela zake nyingi sana. Mimi ndiyo nilimsaidia sasa nashangaa anasema nimemtapeli zaidi ya bilioni. Hivi ningekuwa na zaidi ya bilioni ningekuwa hivi kweli,” alisema Kanyani.

Kanyani ametoa kauli hii baada ya Tanzania PANORAMA Blog kuripoti kuwa amemfilisi Kibombe baada ya kumtaka ampatie Shilingi bilioni 1.4 ili yeye ampatie maboksi yaliyojaa Dola za Marekani ambazo angeziingiza kwenye biashara zake zingeongezeka kimiujiza na hivyo kumpatia utajiri wa haraka zaidi ya ule aliokuwa nao.

  


 

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

SOMA HIYO! ISRAEL NDIYO WAASISI WA MIKWAJU YA PENALTI

LONDON, Uingereza NI jioni ya Agosti 5, 1970 kwenye Uwanja wa Boothferry Park mjini Hull, Manchester United ikiwa ugenini...

AMEJIPATA! LAMPARD ALIVYOREJEA EPL AKIWEKA REKODI

LONDON, Uingereza IKIWA ni miezi 18 tu imepita tangu alipoajiriwa, Frank Lampard ameiwezesha Coventry City kupanda daraja na kurejea...

USICHUKULIE POA! PATORANKING ALIUZA SUMU YA PANYA MITAANI KABLA YA ‘KUTOBOA’

LAGOS, Nigeria WAHENGA walisema maisha ni safari yenye milima na mabonde. Kwamba katika kuishi kwako, si nyakati zote zitakuwa...

KIFO CHA BOSI KINAVYOITESA LEICESTER CITY

LONDON, UingerezaMIAKA 10 iliyopita, Leicester City waliishangaza dunia walipotwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya England (EPL) mbele ya...