Thursday, June 19, 2025
spot_img

MAJALIWA AITAKA TARURA KUWASHIKA MKONO WAHANDISI WAZAWA

RIPOTA WA WAZIRI MKUU

WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa ameitaka Wakala wa Barabara Vijijini na Mijini (TARURA) kuchukua hatua za makusudi za kuwashirikisha wahandisi wazawa kwenye ujenzi wa miradi nchini.

Agizo hilo alilitoa Septemba 14, 2023 alipomuwakilisha Rais Samia Suluhu Hassan kwenye maadhimisho ya siku wahandisi yaliyofanyika katika ukumbi wa Mlimani City, Jijini Dar es Salaam.

Alisema kwa kuzingatia utekelezaji wa mpango wa tatu wa maendeleo wa miaka mitano unaolenga kupunguza ukosefu wa ajira kutoka asilimia tisa hadi nane ifikapo 2025/26, Serikali inatarajia kutimiza azma yake ya kuzingatia ushiriki wa Watanzania kwenye sekta ya ujenzi ili kukuza ujuzi. 

ā€œWizara ya Ujenzi pamoja na bodi ya wahandisi inalifanyia kazi suala la ushiriki mdogo wa wazawa katika miradi ya maendeleo. Hii ni changamoto ambayo mmeiibua, Serikali sasa imeliweka kwenye mpango wa kuhakikisha changamoto hii inafanyiwa kazi ili kuongeza idadi ya wazawa kushiriki katika kazi za ndani,ā€ alisema.

Majaliwa aliesema Serikali imedhamiria kuwawezesha wahandisi wazawa kunufaika na utekelezaji wa miradi mbalimbali inayotekelezwa  nchini.

ā€œMiradi hii ni fursa kwenu, natoa rai mjipange na muwe na juhudi za makusudi kila mmoja kwenye eneo lake ahakikishe kwa uzalendo alionao na mapenzi kwa nchi yake kuwa kinara katika sekta unayosimamia ili kulijenga taifa letu,ā€ alisema.

Aidha, aliielekeza Bodi ya Usajili wa Wahandisi iandae mpango mahususi wa kuwaendeleza wahandisi wanawake ili waweze kusajiliwa kwa wingi zaidi wanapohitimu masomo na kusititiza agizo lake hilo litekelezwe kwa ushirikiano na wadau wengine wa uhandisi.

Naye Naibu Waziri wa Ujenzi, Mhandisi Godfrey Kasekenye alisema Serikali inatambua mchango wa taaluma ya uhandisi katika sekta mbalimbali za kiuchumi kupitia uanzishaji wa viwanda, uendelezaji wa miundombinu ya kilimo, nishati, maji, uvuvi, utumiaji mzuri wa rasilimali na malighafi, usafiri na mawasiliano

ā€œMwaka 2023/2024, Serikali imetenga miradi maalumu ya ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami kwa ajili ya wakandarasi wanawake ambao zabuni zitashindanishwa kwa wakandarasi wanawake tu,ā€ alisema. 

Kwa upamde wake Mwenyekiti wa Bodi ya Usajili wa Wahandisi, Mhandisi Menye David Manga alisema bodi inatarajia kufanya mageuzi ya teknolojia ili kuhakikisha wahandisi waliosajiliwa na wenye sifa wanakuwepo wa kutosha kwa ajili miradi mbalimbali nchini ili kujenga dhana halisi ya ushirikishwaji wa wazawa.

Nyingine Zinazohusiana na Hii

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Tufuatilie

0FansLike
3,913FollowersFollow
0SubscribersSubscribe
- Advertisement -spot_img

Habari Nyingine Mpya