DC MURO 'AJIPIGAPIGA' KIFUA UJENZI WA MADARASA, MAFANIKIO YA ELIMU ARUMERU

Date:

Share post:

 

NA MWANDISHI WETU, ARUMERU

MKUU wa Wilaya ya Arumeru mkoani Arusha (DC) Jerry Murro amesimama mbele ya wananchi wa Wilaya ya Arumeru na kujipigapiga kifua akijivunia mafanikio makubwa yaliyofikiwa na wilaya yake katika sekta ya elimu.

Mbele ya wazazi wa wanafunzi, wadau wa elimu na wafadhili, DC Murro amesema Wilaya ya Arumeru kwa kipindi cha miaka miwili imeendesha kwa mafanikio makubwa kampeni ya ujenzi wa vyumba vya madarasa kwa shule za sekondari na msingi na kwamba Mkoa wa Arusha unajivunia kushika nafasi ya pili kwa ufaulu wa wanafunzi waliomaliza elimu ya msingi.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa awamu ya pili ya ujenzi wa vyumba vya madarasa vya shule za sekondari na msingi wilayani Arumeru, DC Murro amesema yeye mwenyewe pamoja na wananchi wa Arumeru hawana rekodi ya kushindwa kutekeleza maagizo ya viongozi wakuu wa serikali na historia ya wana Arumeru inasomeka vizuri katika utoaji elimu bora na ujenzi wa miundombinu yake.

“Mkoa wetu wa Arusha umekuwa wa pili kitaifa kwa ufaulu wa wanafunzi na sisi kama Mkoa wa Arusha na Wilaya ya Arumeru tumekuwa na ajenda endelevu ya kuhakikisha tunawapokea wanafunzi wote ambao juzi wametangazwa na Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Selemani Jaffo.

” Ndugu zangu wazazi nipo hapa kwanza kiwashukuru kwa kuitikia kampeni yetu ya ujenzi wa vyumba vya madarasa vya shule za msingi na sekondari… Sisi kama Wilaya ya Arumeru tulifanya kazi hiyo kwa miaka miwili mfululizo hivyo hatukuwa na uhaba wa vyumba vya madarasa.

” Tumeanza kampeni ya awamu nyingine ya pili ya ujenzi wa vyumba vinne vya madarasa kwa shule za msingi na sekondari. Sisi Wilaya ya Arumeru mpango wa kujenga vyumba vingine vya madarasa uwe umekamilika kabla ya Februari 22, 2021,” alisema DC Murro.

Mkuu huyo wa wilaya anaendelea na kampeni ya kuhamasisha ujenzi wa madarasa kwa wilaya za Meru na Arumeru ikiwa ni utekelezaji wa agizo la Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa linalowataka viongozi wenye dhamana ya kusimamia sekta ya elimu kuhahakisha wanafunzi wote wanaoanza elimu ya msingi na waliochaghuliwa kujiunga kidato cha kwanza hawakosi madarasa na madawati.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

NEWCASTLE KUMUUZA MSHAMBULIAJI WA BEI MBAYA

LONDON, UingerezaKLABU ya Newcastle United itampiga bei straika raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), Yoane Wissa,...

LIVERPOOL NAYO YAJITOSA KWA WHARTON

MERSEYSIDE, UingerezaLIVERPOOL imeungana na klabu zingine kubwa za Ulaya zinazomtolea macho kiungo wa Crystal Palace, Adam Wharton. Mtandao wa...

SINTOFAHAMU KUELEKEA MAZUNGUMZO YA PILI KATI YA MAREKANI, IRAN

WASHINGTON DC, MarekaniAKIZUNGUMZA na waandishi wa habari Aprili 16, 2026, Rais wa Marekani, Donald Trump, alisema ana matumaini...

TAJIRI WA MAN CITY ANAHUSIKA VIPI VITA NCHINI SUDAN?

MANCHESTER, UingerezaMMILIKI wa klabu ya Manchester City, Sheikh Mansour bin Zayed Al-Nahyan, anakabiliwa na tuhuma nzito za kusambaza...