WAZIRI AWATAKA UHAMIAJI KUIMARISHA USALAMA MIPAKANI

Date:

Share post:

MWANDISHI MAALUMU

LOLIONDO.

WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi. Hamad Yusufu Masauni ameitaka Idara ya Uhamiaji nchini kusimamia uingiaji na utokaji wa wageni katika mipaka ya nchi kwa kufuata sheria za nchi.

Waziri Masauni aliyasema hayo mapema wiki hii akiwa Ngorongoro mkoani Arusha alikokwenda  kukagua maendeleo ya kazi ya uwekaji wa alama za mipaka katika eneo la Pori Tengefu la Loliondo.

Aidha, Masauni alibainisha kuwa Serikali itafanya uhakiki wa kina kubaini uendeshaji wa asasi za kiraia nchini kufanya kazi zao kwa mujibu wa sheria na zile zitakazokiuka zitachukuliwa hatua kali za kisheria.

Masauni alieleza kuridhishwa kwake na maendeleo ya kazi na kuwataka wahusika kuhakikisha kuwa kazi hiyo inakamilika kwa wakati.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Ngorongoro Mwalimu Raymond Mangwala aliyemwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Arusha, John Mongela, alimueleza Waziri Masauni kuwa amepokea maelekezo yake na atahakikisha hali ya usalama wa wananchi na mali zao inaendelea kuimarishwa wilayani Ngorongoro na kuwa kazi  hiyo itaendelea kwa hali ya amani  na utulivu.



 

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

KIFO CHA BOSI KINAVYOITESA LEICESTER CITY

LONDON, UingerezaMIAKA 10 iliyopita, Leicester City waliishangaza dunia walipotwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya England (EPL) mbele ya...

ISHU YA RASHFORD BADO PASUA KICHWA

MANCHESTER, UingerezaKOCHA wa Manchester United, Michael Carrick, amesema bado haijafahamika kama Marcus Rashford atarudi klabuni hapo au atabaki...

BARCA YAPATA MRITHI WA LEWANDOWSKI

CATALUNYA, HispaniaKLABU ya Barcelona imeanza mipango ya kumsajili mshambuliaji wa kati wa Real Mallorca, Vedat Muriqi, ikiamini anatosha...

ARSENAL AKILI YOTE KWA MONGA

LONDON, UingerezaARSENAL ya Kaskazini mwa Jiji la London imeonesha nia ya kumsajili winga anayefanya vizuri Ligi Daraja la...