DENDEGO: CHANGAMKIENI FURSA ZA UTALII

Date:

Share post:

RIPOTA PANORAMA

MKUU wa Mkoa wa Iringa, Halima Dendego amewataka wakazi wa mkoa huo kuchangamkia fursa za utalii kufuatia Kongamano la Kimataifa la Utalii litakalofanyika katika viwanja vya Kihesa Kilolo.

Kongamano hilo litakaloanza Novemba 9-13 limelenga kufungua milango ya utalii Kusini mwa Tanzania na kutangaza vivutio vya utalii vinavyopatikana katika mikoa 10.

Mikoa inayoshiriki kongamano hilo ni Iringa, Mbeya, Katavi, Rukwa, Ruvuma, Mtwara, Lindi, Njombe, Songwe na Morogoro.
Akizungumza na wanahabari mkoani Iringa, Dendego amesema hiyo ni nafasi adhimu kwa wakazi wa Mkoa wa Iringa kuchangamkia fursa za kiutalii.

Amesema wananchi wanaweza kutumia kongamano hilo kuuza bidhaa zao mbalimbali ikiwemo vyakula.

“Hili ni kongamano lenye hadhi ya Kimataifa kwa hiyo Changamkieni huu fursa,uwe mfanyabiashara mdogo au mkubwa nafasi ipo,” amesema Dendego.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Makumbusho ya Mkoa wa Iringa, Jimson Sanga amesema kongamano hilo litasaidia kukuza sekta ya utalii kwenye mikoa hiyo.

Amesema pia litaongeza ari ya wageni kutembelea vivutio vya kitalii vinavyo patikana katika mikoa hiyo.

About The Author

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

USIYOYAJUA KUHUSU KOCHA ALIYEANDIKA HISTORIA BUNDESLIGA

MUNICH, Ujerumani JINA la Marie-Louise Eta limeandika historia katika soka la Ujerumani baada ya kuwa mwanamke wa kwanza kuwa...

BURNA BOY HATAKI MAZOEA, ‘BIFU’ KWAKE KAWAIDA TU

HIVI karibuni, supastaa wa muziki wa Afrobeat, Burna Boy, aliingia kwenye mikono ya Chama cha 'Ma-dj' nchini Nigeria,...

BURKINA FASO IKO HOI AU HAI CHINI YA KAPTENI TRAORE?

HATUA ya kutangaza kuwa raia wake waaitarajie demokrasia imeibua maswali mengi juu ya uongozi wa Kapteni Ibrahim Traore...

SIMU YAKO CHANZO CHA UGONJWA WA MOYO, SARATANI?

UKWELI ulio wazi ni kwamba matumizi ya simu za mkononi yameongezeka kwa kasi duniani, Tanzania ikiwa na 'laini'...