SAMIA AONYA UDOKOZI MIRADI YA UMMA

Date:

Share post:

RIPOTA PANORAMA

RAIS Samia Suluhu Hassan amewataka Watanzania watakaopata fursa za ajira katika ujenzi wa uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Msalato jijini hapa kuepuka udokozi.

Rais Samia ameyasema hayo leo Jumapili Oktoba 30, 2022, wakati wa hafla ya uwekaji wa jiwe la msingi katika ujenzi wa uwanja huo.

Rais Samia amesema mradi huo ni mali ya Watanzania na wakazi wa Dodoma wote.

Rais Samia amewaomba Watanzania kutohujumu mradi huo na badala yake kuwa walinzi wake.

“Wakati mwingine mnapata ajira katika miradi hii lakini mnatabia ya mkono, mkono, kuondoka na mifuko ya saruji, kuondoka na kifuko cha misumari, kipande cha nondo.

“Niombe sana mtakaopata ajira hapa, twendeni tuwajibike ipasavyo ili mradi ukamilike Desemba 2024 wakati ,”amesema.

Amesema ujenzi wa viwanja vya ndege umepewa kipaumbele katika sera ya usafiri nchini ambapo kila mkoa unatakiwa kuwa na kiwanja cha ndege chenye uwezo wa kuhudumia ndege zinazobeba si chini ya abiria 70.

Amesema pamoja na uwanja wa ndege wa Msalato kuna viwanja vya ndege vingine vinaendelea kujengwa nchini.

Rais Samia amesema lengo lao ni kukuza biashara katika ukanda wa Afrika Mashariki.

About The Author

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

USIYOYAJUA KUHUSU KOCHA ALIYEANDIKA HISTORIA BUNDESLIGA

MUNICH, Ujerumani JINA la Marie-Louise Eta limeandika historia katika soka la Ujerumani baada ya kuwa mwanamke wa kwanza kuwa...

BURNA BOY HATAKI MAZOEA, ‘BIFU’ KWAKE KAWAIDA TU

HIVI karibuni, supastaa wa muziki wa Afrobeat, Burna Boy, aliingia kwenye mikono ya Chama cha 'Ma-dj' nchini Nigeria,...

BURKINA FASO IKO HOI AU HAI CHINI YA KAPTENI TRAORE?

HATUA ya kutangaza kuwa raia wake waaitarajie demokrasia imeibua maswali mengi juu ya uongozi wa Kapteni Ibrahim Traore...

SIMU YAKO CHANZO CHA UGONJWA WA MOYO, SARATANI?

UKWELI ulio wazi ni kwamba matumizi ya simu za mkononi yameongezeka kwa kasi duniani, Tanzania ikiwa na 'laini'...