UKAME WAKWAMISHA UWEKAJI MIFUGO HERENI

Date:

Share post:

RIPOTA PANORAMA

UWEKAJI hereni za kieletroniki kwa mifugo kwenye wilaya za Mkoa wa Arusha halitafanikiwa kwa sababu ya ukame unaozikabili wilaya mbalimbali na kusababisha mifugo kupelekwa mikoa ya Tanga, Manyara na hata Kenya kwa ajili ya kutafuta malisho

Akizungumza jana katika kikao cha Kamati ya Ushauri Mkoa wa Arusha (RCC), Naibu Waziri wa  Madini, Dk,Steven Kiruswa,  alisema suala hilo halitafanikiwa na kuiomba Wizara ya Mifugo na Uvuvi kuongeza muda zaidi badala ya kuisha Oktoba 31,mwaka huu.

Amesema ukame umesababisha wafugaji kuhama na mifugo, wengine kuipeleka Kenya,Tanga ,Manyara na mikoa mbalimbali, ili iweze kupata malisho na maji kutokana na janga la ukame, hivyo kwa wafugaji ambao wamehama maeneo yao halitafanikiwa kama wizara iangalie jambo hilo.

Wizara ya Mifugo na Uvuvi, ilitangaza suala la utambuzi wa mifugo kwa kutumia hereni za kieletroniki kumalizika Oktoba 31 mwaka huu, baada ya hapo wafugaji watatozwa faini.

About The Author

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

USIYOYAJUA KUHUSU KOCHA ALIYEANDIKA HISTORIA BUNDESLIGA

MUNICH, Ujerumani JINA la Marie-Louise Eta limeandika historia katika soka la Ujerumani baada ya kuwa mwanamke wa kwanza kuwa...

BURNA BOY HATAKI MAZOEA, ‘BIFU’ KWAKE KAWAIDA TU

HIVI karibuni, supastaa wa muziki wa Afrobeat, Burna Boy, aliingia kwenye mikono ya Chama cha 'Ma-dj' nchini Nigeria,...

BURKINA FASO IKO HOI AU HAI CHINI YA KAPTENI TRAORE?

HATUA ya kutangaza kuwa raia wake waaitarajie demokrasia imeibua maswali mengi juu ya uongozi wa Kapteni Ibrahim Traore...

SIMU YAKO CHANZO CHA UGONJWA WA MOYO, SARATANI?

UKWELI ulio wazi ni kwamba matumizi ya simu za mkononi yameongezeka kwa kasi duniani, Tanzania ikiwa na 'laini'...