MADIWANI MPIMBWE WAHOJI UJENZI WA BARABARA

Date:

Share post:

RIPOTA PANORAMA

BARAZA la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Mpimbwe, Mkoa wa Katavi, limemtaka Meneja wa wakala wa Barabara za Mijini na Vijijini (TARURA), kuhakikisha anashughulikia barabara zote zinazotakiwa kutengenezwa.

Wakichangia taarifa ya utekelezaji wa barabara iliyowasilishwa na Meneja wa TARURA Wilaya ya Mlele, Mhandisi Maneno Makorongo juu ya ukarabati wa barabara za halmashauri hiyo, madiwani wamesema inasikitisha kuona barabara zinashindwa kukamilika kukamilika kwa wakati na nyingine hata hazijaanza ujenzi.

Awali akitoa ufafanuzi, Mhandisi Makorongo amesema tatizo la kuchelewa kukarabatiwa barabara hizo ni changamoto ya uhaba wa wakandarasi, jambo ambalo lilipingwa na Mwenyeketi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpimbwe, Sailas Irumba.

“Kila siku mkandarasi, mkandarasi. Meneja sisi hatutaki hao wakandarasi, nchi hii ina wakandarasi wengi tunataka wananchi wetu Halmashauri ya Mpimbwe waweze kuneemeka na fedha anayoitoa Mheshimiwa Rais kwenye TARURA,”amesema.

Baada ya Mwenyekiti kutoa kauli hiyo, Mhandisi Makorongo aliwaahidi madiwani kuwa atazingatia ushauri uliotolewa na kuufanyia kazi.

About The Author

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

USIYOYAJUA KUHUSU KOCHA ALIYEANDIKA HISTORIA BUNDESLIGA

MUNICH, Ujerumani JINA la Marie-Louise Eta limeandika historia katika soka la Ujerumani baada ya kuwa mwanamke wa kwanza kuwa...

BURNA BOY HATAKI MAZOEA, ‘BIFU’ KWAKE KAWAIDA TU

HIVI karibuni, supastaa wa muziki wa Afrobeat, Burna Boy, aliingia kwenye mikono ya Chama cha 'Ma-dj' nchini Nigeria,...

BURKINA FASO IKO HOI AU HAI CHINI YA KAPTENI TRAORE?

HATUA ya kutangaza kuwa raia wake waaitarajie demokrasia imeibua maswali mengi juu ya uongozi wa Kapteni Ibrahim Traore...

SIMU YAKO CHANZO CHA UGONJWA WA MOYO, SARATANI?

UKWELI ulio wazi ni kwamba matumizi ya simu za mkononi yameongezeka kwa kasi duniani, Tanzania ikiwa na 'laini'...