PANYA WATEKETEZA MASHAMBA KILOMBERO

Date:

Share post:

RIPOTA PANORAMA

PANYA wameteketeza alizeti na mahindi yaliyokuwa yanakaribia kuvunwa katika mashamba yenye jumla ya hekta 90.5 Kata ya Chita, Wilaya ya Kilombero mkoani Morogoro.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, Bwana Shamba wa Kata hiyo, Philbert Lawrent, amesema tatizo la panya hao limekuwa kubwa katika vijiji viwili vya Chita na Makutano, kati ya vitano vilivyopo.

Amesema wamekuwa wakifanya jitihada za kuwadhibiti panya hao kwa kutumia njia za kienyeji pamoja na sumu.

Ametaja njia hizo kuwa ni kuchimbia ndoo chini na kuweka maji kisha kuzungushia pumba pamoja na kupurua miti ya mahindi, ili panya hao washindwe kupanda.

Amesema kwa kuwa tatizo ni kubwa wakulima hao wanaweza wasiambulie hata kidogo mazao waliyoyapanda.

Mkulima Hedrick Magome aliyelima alizeti na mahindi katika Kata ya Chita, amesema amelima eka sita mahindi ambayo yamefikia hatua ya kuchomwa na alizeti hatua ya kuchanua, kisha wakazuka panya kwa wingi walioanza kula mazao hayo.

” Kwa kipindi cha wiki moja wameshambulia mahindi nimeambulia kuvuna machache, ambayo ni mabichi ambayo nimewapa nguruwe, nasi tumetumia na majirani,” amesema.

Kwa maelezo yake walipoanza kula alizeti alinunua sumu lakini haikusaidia kutokana na wingi wa panya hao.

” Nilishauriwa ninunue ndoo za lita 20 nichimbie chini na kuweka maji nusu kisha nizungushie pumba, ikiwa ni njia ya kuwatega panya hao, nilinunua majaba na kuchimbia, Siku ya kwanza nilitoa panya 200, kila siku waliongeza hadi kufikia 1000 kwa siku,” amesema.

Ameongeza kuwa hivi sasa hata kuwatoa anaona kinyaa wamenaswa wengi, hivyo ameamua kuwaacha.

Amesema panya hao walianza mashambulizi mwishoni mwa Agosti mwaka huu, amejitahidi kuwadhibiti bila mafanikio.

About The Author

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

USIYOYAJUA KUHUSU KOCHA ALIYEANDIKA HISTORIA BUNDESLIGA

MUNICH, Ujerumani JINA la Marie-Louise Eta limeandika historia katika soka la Ujerumani baada ya kuwa mwanamke wa kwanza kuwa...

BURNA BOY HATAKI MAZOEA, ‘BIFU’ KWAKE KAWAIDA TU

HIVI karibuni, supastaa wa muziki wa Afrobeat, Burna Boy, aliingia kwenye mikono ya Chama cha 'Ma-dj' nchini Nigeria,...

BURKINA FASO IKO HOI AU HAI CHINI YA KAPTENI TRAORE?

HATUA ya kutangaza kuwa raia wake waaitarajie demokrasia imeibua maswali mengi juu ya uongozi wa Kapteni Ibrahim Traore...

SIMU YAKO CHANZO CHA UGONJWA WA MOYO, SARATANI?

UKWELI ulio wazi ni kwamba matumizi ya simu za mkononi yameongezeka kwa kasi duniani, Tanzania ikiwa na 'laini'...