‘WANASIASA MWACHENI AKWILINA APUMZIKE KWA AMANI’

Date:

Share post:

RIPOTA PANORAMA

WANASIASA wameonywa kuutumia kisiasa msiba wa mwanafunzi Akwilina Akwilini na badala yake wametakiwa kumuacha apumzike kwa amani.

Akwilina aliuawa mwezi uliopita baada ya kupigwa risasi wakati polisi wakitawanya maandamano ya wanachama na mashabiki wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)

Mbali na wanasiasa, wengine walioonywa kuacha kuutumia msiba huo kwa malengo yao ni makundi ya wanaharakati yanayotumia mwamvuli wa wanasiasa.

Onyo hili limetolewa jana na Mwenyekiti Jumuiya ya Taasisi za Vyuo vya Elimu ya Juu Tanzania (TAHLISO), George Mnali katika mkutano wa kamati tendaji ya umoja huo. Kamati hiyo iliketi jana kujadili changamoto zinazowakabili wanafunzi wa vyuo vikuu.

Mnali alisema TAHLISO inaelekeza lawama kwa makundi matatu kwa tukio hilo aliyoyataja kuwa ni wanasiasa, wananchi na waliozuia maandamano hayo ambayo yaligharimu uhai wa Akwilina.

Alisema wanasiasa wanapaswa kuchunga kauli zao, waangalie wanazungumza nini na wapi kwa sababu Taifa linataka amani.

Mnali alisema onyo hilo halilenga kundi lolote la wanasiasa bali linawahusu wote na kwamba waliozuia maandamano na kuibua ghasia walipaswa kuwa makini kwa sababu katika maandamano yale kilichotakiwa ni kuzuia tu.

“TAHLISO ndio chombo kikuu cha kuwasemea wanafunzi wote nchi nzima, hakuna mwingine. Tambua kuna kifo cha mwanafunzi mwenzetu Akwilina aliyekuwa anasoma Chuo cha Usafirishaji lakini kuna vikundi vimejitokeza kutoa matamko mbalimbali.

“Vikundi vingine vimeenda mbali zaidi kwa kuwataka baadhi ya watendaji kujiuzulu wakati uchunguzi bado unaendelea na matokeo
hayajatoka, inaashiria vinatumika kisiasa,” alisema Mnali

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

KIFO CHA BOSI KINAVYOITESA LEICESTER CITY

LONDON, UingerezaMIAKA 10 iliyopita, Leicester City waliishangaza dunia walipotwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya England (EPL) mbele ya...

ISHU YA RASHFORD BADO PASUA KICHWA

MANCHESTER, UingerezaKOCHA wa Manchester United, Michael Carrick, amesema bado haijafahamika kama Marcus Rashford atarudi klabuni hapo au atabaki...

BARCA YAPATA MRITHI WA LEWANDOWSKI

CATALUNYA, HispaniaKLABU ya Barcelona imeanza mipango ya kumsajili mshambuliaji wa kati wa Real Mallorca, Vedat Muriqi, ikiamini anatosha...

ARSENAL AKILI YOTE KWA MONGA

LONDON, UingerezaARSENAL ya Kaskazini mwa Jiji la London imeonesha nia ya kumsajili winga anayefanya vizuri Ligi Daraja la...