MILIONI 18 ZAMLIZA MBUNGE WA CCM

Date:

Share post:

RIPOTA PANORAMA

MBUNGE wa Viti Maalumu wa Mkoa wa Iringa, Rose Tweve leo amelia machozi hadharani baada ya kupewa Shilingi milioni 18 kwa ajili ya mradi ya maendeleo ya akina mama.

Tweve amepewa fedha hizo na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Salimu Asas mbele ya wajumbe wa Baraza za Wanawake (UWT) la CCM, Wilaya ya Mufindi ukiwa ni mchango wake kwa ajili ya miradi ya maendeleo ya akina mama.

Asas aliamua kutoa fedha hizo kumuunga mkono Tweve ambaye aliyetoa Sh. 600,000 kwa kata 17 za wilaya hiyo kwa ajili ya kuinua uchumi wa wananchi.

Imeelezwa kuwa lengo Tweve ni kutoa Sh. Milioni 60 kwa kata zote za Mkoa wa Iringa.

Assas baada ya kutoa kiasi hicho cha fedha alisema amefurahishwa na mkakati wa Tweve wa kuwafikia wananchi wa kipato cha chini wanaostahili kuinuliwa kiuchumi.

Tweve baada ya kupokea fedha hizo huku machozi yakimbubujika alisema anajisikia furaha na amani kuona watu wanathamini mchango wake katika jamii na kumuunga mkono

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

KIFO CHA BOSI KINAVYOITESA LEICESTER CITY

LONDON, UingerezaMIAKA 10 iliyopita, Leicester City waliishangaza dunia walipotwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya England (EPL) mbele ya...

ISHU YA RASHFORD BADO PASUA KICHWA

MANCHESTER, UingerezaKOCHA wa Manchester United, Michael Carrick, amesema bado haijafahamika kama Marcus Rashford atarudi klabuni hapo au atabaki...

BARCA YAPATA MRITHI WA LEWANDOWSKI

CATALUNYA, HispaniaKLABU ya Barcelona imeanza mipango ya kumsajili mshambuliaji wa kati wa Real Mallorca, Vedat Muriqi, ikiamini anatosha...

ARSENAL AKILI YOTE KWA MONGA

LONDON, UingerezaARSENAL ya Kaskazini mwa Jiji la London imeonesha nia ya kumsajili winga anayefanya vizuri Ligi Daraja la...