OKELLO NAMBA ZINAONGEA LIGI KUU BARA

Date:

Share post:

MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Uganda, Allan Okello, amethibitisha kuwa Yanga haikufanya makosa kumsajili wakati wa dirisha dogo lililopita.

Okello alisajiliwa Januari, 2026, wakati wa usajili wa dirisha dogo, akitokea Ligi Kuu ya Uganda alikokuwa akiitumikia Vipers.

Licha ya kusuasua katika siku zake za mwanzo, hata baadhi ya mashabiki kubeza uwezo wake, nyota huyo ameamka na kuonesha makali yake katika mechi za Ligi Kuu Bara alizocheza hivi karibuni.

Iko hivi; katika michezo mitatu ya Ligi iliyopita, Okello, ambaye pia ni tegemeo kwenye timu yake ya Taifa ya Uganda ‘The Crane’, ametoa pasi za mabao (asisti) sita.

Aprili 4, 2026, katika mchezo dhidi ya Prisons, Yanga ilishinda mabao 3-0, huku Okello akifunga dakika ya 50 na kutoa asisti kwa Mudathir Yahya (dk. 68).

Aprili 8, 2026, wakati Yanga ilipoifunga Pamba Jiji mabao 3-0, alitoa asisti kwa wafungaji wote; Mudathir (dk. 9 na dk. 34) na Maxi Nzengeli (dk. 68).

Aprili 16, 2026, Okello alipiga asisti kwa Ngezeli (dk. 6) na Mohamed Hussein ‘Tshabalala’ (dk. 45) wakati Yanga ikiibuka na ushindi wa mabao 6-0.

Huyo ndiye Okello ‘Star Boy’, akitajwa kuwa miongoni mwa vipaji vikubwa katika soka la Uganda kwa sasa.

About The Author

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

VIONGOZI LONGIDO WATAKIWA KUHARAKISHA UANZISHAJI WA JUHIZINA

Viongozi wa vijiji katika Halmashauri ya Wilaya ya Longido wametakiwa kuongeza kasi ya utekelezaji wa mchakato wa kuanzisha...

LIGI YA EUROPA KUMEKUCHA NUSU FAINALI

LONDON, UingerezaMECHI za marudiano hatua ya robo fainali ya msimu huu wa Ligi ya Europa zilimalizika usiku wa...

MAZUNGUMZO YA ISRAEL, LEBANON KUITULIZA HEZBOLLAH?

BEIRUT, LebanonRAIS wa Marekani, Donald Trump, ameutangazia ulimwengu kuwa viongozi wa Israel na Lebanon wameifikia makubaliano ya kusitisha...

MTANDA AKUTANA NA UONGOZI NA JMAT, KUWAASA USHIRIKIANO NA AMANI

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Said Mtanda, amekutana na kufanya mazungumzo na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Maridhiano...