MTANDA AIPONGEZA REA KWA KUFIKISHA UMEME VIJIJINI MWANZA

Date:

Share post:

Leo April 16 Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Said Mtanda, ameipongeza Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa utekelezaji wa miradi ya umeme vijijini kwa ufanisi, hatua iliyowezesha upatikanaji wa huduma hiyo katika maeneo mengi ya mkoa huo na kuchochea ukuaji wa shughuli za kiuchumi, hususan sekta ya uvuvi.

Mhe. Mtanda alitoa pongezi hizo alipokutana na uongozi wa REA uliofika ofisini kwake kwa ajili ya mazungumzo, ikiwa ni sehemu ya ziara ya kutembelea miradi ya nishati pamoja na kushiriki mkutano wa washirika wa maendeleo ya nishati (RDPG).

Alieleza kuwa uchumi wa Mkoa wa Mwanza unategemea kwa kiasi kikubwa shughuli za uvuvi, na kwamba juhudi za REA kusambaza umeme pamoja na kutoa taa maalum zinazotumia nishati ya jua kwa ajili ya uvuvi wa dagaa zimekuwa msaada mkubwa, hasa katika uvuvi wa nyakati za usiku.

Aidha, Mhe. Mtanda alibainisha kuwa bado kuna visiwa na vitongoji ambavyo havijafikiwa na huduma ya umeme, lakini akasisitiza kuwa juhudi zinaendelea kuhakikisha maeneo hayo yanaunganishwa na nishati hiyo muhimu.

“Nawapongeza sana REA kwa kazi kubwa mnayoifanya. Hakuna ubaguzi katika utoaji wa huduma zenu kwani mnawahakikishia wananchi wote wanapata umeme, jambo linalochochea shughuli za uzalishaji.

Nawashukuru pia kwa kuwafikia wafugaji wetu, ikiwemo mfugaji tuliyemtembelea leo mwenye zaidi ya kuku 30,000,” alisema Mhe. Mtanda.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Bodi ya REA, Balozi Meja Jenerali (Mstaafu) Jacob Kingu, aliwashukuru washirika wa maendeleo kwa mchango wao katika upatikanaji wa nishati vijijini.

Alisema ushirikiano huo umewezesha wananchi wengi kunufaika na huduma ya umeme pamoja na kuanzisha miradi mbalimbali ya kiuchumi.

Aliongeza kuwa REA itaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali kuhakikisha huduma ya umeme inawafikia wananchi wote, ikiwa ni sehemu ya kuchochea maendeleo ya kijamii na kiuchumi nchini.

About The Author

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

UCHUMI WA CHINA WAZIDI KUIMARIKA

BEIJING, China LICHA ya vita vya Marekani na Iran kuonekana kuitikisa dunia, China imeendelea kupiga hatua kubwa katika eneo...

SIKU 100 ZA RAIS MPYA WA VENEZUELA: MABADILIKO NA MASWALI MAPYA

CARACAS, Venezuela BAADA ya vikosi vya Marekani kumng’oa madarakani aliyekuwa Rais wa Venezuela, Nicolás Maduro kwenye oparesheni ya Januari...

MAELFU YA FAMILIA SUDAN BADO WAKIMBIA VITA, HALI YA MAISHA YAZIDI KUWA MBAYA

MAELFU ya familia nchini Sudan bado wanalazimika kuyakimbia makazi yao, miji na hata mipaka ya nchi kufuatia vita...

ISRAEL YAENDELEA NA OPERESHEN DHIDI YA HEZBOLLAH NCHINI LEBANON

Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu amesema Jeshi la nchi yake linaendelea na operesheni dhidi ya wanamgambo wanaoungwa...