NANE WAOKOLEWA NA JESHI LA ZIMAMOTO KWENYE MAFURIKO KILIMANJARO

Date:

Share post:

Jeshi la Zimamoto na Uokoaji katika Wilaya ya Siha, mkoani Kilimanjaro, limefanikiwa kuwaokoa watu nane waliokuwa wamezingirwa na maji kufuatia mvua kubwa zilizosababisha mafuriko.

Tukio hilo limetokea leo Aprili 11, 2026 majira ya saa 07:45 asubuhi katika kijiji cha Koboko Kusini, Kata ya Nasai wilayani Siha, baada ya maji kuingia kwenye makazi ya wananchi na kuwazuia kutoka nje.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka kituo cha Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Siha, askari walifika eneo la tukio kwa wakati na kuanza operesheni ya uokoaji, ambapo walifanikiwa kuwaokoa watu wote waliokuwa wamekwama ndani ya nyumba zilizozingirwa na maji.

Waliookolewa ni watu wazima wawili pamoja na watoto sita, wote wakiwa wa jinsia ya kike. Aidha, watu wengine wanne waliripotiwa kuathirika na tukio hilo.

About The Author

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

USIYOYAJUA KUHUSU KOCHA ALIYEANDIKA HISTORIA BUNDESLIGA

MUNICH, Ujerumani JINA la Marie-Louise Eta limeandika historia katika soka la Ujerumani baada ya kuwa mwanamke wa kwanza kuwa...

BURNA BOY HATAKI MAZOEA, ‘BIFU’ KWAKE KAWAIDA TU

HIVI karibuni, supastaa wa muziki wa Afrobeat, Burna Boy, aliingia kwenye mikono ya Chama cha 'Ma-dj' nchini Nigeria,...

BURKINA FASO IKO HOI AU HAI CHINI YA KAPTENI TRAORE?

HATUA ya kutangaza kuwa raia wake waaitarajie demokrasia imeibua maswali mengi juu ya uongozi wa Kapteni Ibrahim Traore...

SIMU YAKO CHANZO CHA UGONJWA WA MOYO, SARATANI?

UKWELI ulio wazi ni kwamba matumizi ya simu za mkononi yameongezeka kwa kasi duniani, Tanzania ikiwa na 'laini'...