KAMATI YA YAFANYA UKAGUZI WA MIRADI YA MAENDELEO MTAMA

Date:

Share post:

Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira ya Halmashauri ya Wilaya ya Mtama, Aprili 11, 2026, imefanya ziara ya kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa katika halmashauri hiyo kwa lengo la kujionea maendeleo ya ujenzi yanavyoendelea.

Akiongoza ziara hiyo, Mwenyekiti wa Kamati ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Mandwanga, Mhe. Ally Ulaya, ameonesha kuridhishwa na hatua iliyofikiwa katika utekelezaji wa miradi hiyo, huku akimtaka Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri, Ndugu Anderson Msumba, kuongeza juhudi ili miradi hiyo ikamilike kwa wakati uliopangwa.

Amesema kuwa miradi hiyo ina manufaa makubwa kwa wananchi wa Mtama, hususan katika kuboresha huduma za kijamii kama afya, lakini akabainisha kuwa bado kuna haja ya kuongeza kasi ya utekelezaji wake.

“Tumeshuhudia namna miradi hii itakavyowanufaisha wananchi, lakini kasi yake hairidhishi. Ni muhimu kuongeza nguvu ili ikamilike na ianze kutoa huduma,” amesema Mhe. Ulaya.

Aidha, Mhe. Ulaya amesisitiza umuhimu wa kuwawezesha wakandarasi wanaotekeleza miradi hiyo ili waweze kukamilisha kazi kwa ubora na ufanisi, jambo litakalosaidia kudumu kwa muda mrefu na kutoa huduma iliyokusudiwa.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Ndugu Anderson Msumba, amesema halmashauri inaendelea kuchukua hatua mbalimbali za ndani kuhakikisha miradi hiyo inakamilika kwa wakati, ikiwemo kuboresha mifumo ya usimamizi na ufuatiliaji.

Ameongeza kuwa utekelezaji wa miradi hiyo umeanza kuleta mabadiliko chanya katika Wilaya ya Mtama, ikiwemo kuongeza fursa za ajira kwa vijana na kuchochea maendeleo ya kiuchumi katika eneo hilo.

Katika ziara hiyo, Kamati ilitembelea miradi ya ujenzi wa Stendi ya Mabasi ya Mtama pamoja na jengo la mionzi katika Kituo cha Afya Mtama.

About The Author

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

USIYOYAJUA KUHUSU KOCHA ALIYEANDIKA HISTORIA BUNDESLIGA

MUNICH, Ujerumani JINA la Marie-Louise Eta limeandika historia katika soka la Ujerumani baada ya kuwa mwanamke wa kwanza kuwa...

BURNA BOY HATAKI MAZOEA, ‘BIFU’ KWAKE KAWAIDA TU

HIVI karibuni, supastaa wa muziki wa Afrobeat, Burna Boy, aliingia kwenye mikono ya Chama cha 'Ma-dj' nchini Nigeria,...

BURKINA FASO IKO HOI AU HAI CHINI YA KAPTENI TRAORE?

HATUA ya kutangaza kuwa raia wake waaitarajie demokrasia imeibua maswali mengi juu ya uongozi wa Kapteni Ibrahim Traore...

SIMU YAKO CHANZO CHA UGONJWA WA MOYO, SARATANI?

UKWELI ulio wazi ni kwamba matumizi ya simu za mkononi yameongezeka kwa kasi duniani, Tanzania ikiwa na 'laini'...