WATENGENEZA MAUDHUI ARUSHA WAPATIWA MAFUNZO MAALUM YA KUIMARISHA UWEZO WAO.

Date:

Share post:

Watengeneza  maudhui nchini wametakiwa kuzingatia matumizi sahihi ya fedha, kuweka akiba, kusimamia vyema miradi yao pamoja na kujifunza elimu ya uwekezaji ili waweze kujikwamua kiuchumi kupitia mikopo wanayopata kutoka Mfuko wa Utamaduni na Sanaa

Wito huo ulitolewa na Mtendaji Mkuu wa Mfuko wa Sanaa, Utamaduni na Michezo CPA Nyakaho Mahemba, wakati wa mafunzo kwa watengenezaji maudhui ‘content creators’ mkoani Arusha, yaliyofanyika kwenye Hoteli Corido Spring.

Washiriki hao wamehimizwa kuzingatia matumizi ya lugha za kigeni ili kupanua soko la kazi zao kimataifa, kuzingatia maadili ya Kitanzania, kujifunza tabia za wanyama wanapozalisha maudhui, pamoja na kulinda taarifa binafsi kabla ya kuyachapisha.

 Aidha amesisitiza kuwa, Wizara ya Habari, Mishezo, Sanaa na Utamaduni kupitia mfuko huo, haina upendeleo katika utoaji wa mikopo ukiwa na lengo la kuwawezesha watengenezaji maudhui kuinuka kiuchumi kupitia sanaa na vipaji vyao hivyo elimu ya fedha, inahitaji kuwa na utamaduni wa kuweka akiba na kurejesha mikopo kwa wakati ili kukuza taaluma ya sanaa na kuifanya kuwa chanzo endelevu cha ajira na kipato.

“Mfuko wa Utamaduni na Sanaa unatoa mikopo ili kuwawezesha wasanii na watengenezaji maudhui kukua kiuchumi, hivyo ni muhimu kurejesha mikopo hiyo kwa wakati ili kuwapa nafasi wengine kunufaika pia,” . Amebainisha CPA Mahemba

Naye Mhandisi Benezeth Kabundugur,  kutoka Kitengo cha Nishati Safi ya Kupikia aliwataka watengenezaji maudhui kutumia majukwaa yao ya kidijitali kuhamasisha mabadiliko chanya katika jamii, hususan matumizi ya nishati safi ya kupikia.

Amesisitiza kuwa, wanayo nafasi kubwa ya kuelimisha na kuhamasisha jamii matumizi ya nishati safi kwa mbinu zenye mvuto kama video fupi, vichekesho, hadithi na simulizi za maisha halisi ili kufikisha ujumbe kwa ufanisi.

“Mhe. Rais Dkt. Samia ni kinara wa ajenda ya nishati safi ya kupikia barani Afrika, muungeni mkono kwa vitendo ili kufanikisha lengo la kitaifa la kufikia asilimia 80 ya matumizi ya nishati safi ya kupikia ifikapo mwaka 2034″Amesema Kabundugur.

Awali, Mafunzo hayo ya siku moja yameandaliwa na Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa kushirikiana na Mfuko wa Utamaduni na Sanaa Tanzania, huku Wizara ya Nishati ikiwa miongoni mwa wadhamini wakuu pamoja na Benki ya CRDB.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

SOMA HIYO! ISRAEL NDIYO WAASISI WA MIKWAJU YA PENALTI

LONDON, Uingereza NI jioni ya Agosti 5, 1970 kwenye Uwanja wa Boothferry Park mjini Hull, Manchester United ikiwa ugenini...

AMEJIPATA! LAMPARD ALIVYOREJEA EPL AKIWEKA REKODI

LONDON, Uingereza IKIWA ni miezi 18 tu imepita tangu alipoajiriwa, Frank Lampard ameiwezesha Coventry City kupanda daraja na kurejea...

USICHUKULIE POA! PATORANKING ALIUZA SUMU YA PANYA MITAANI KABLA YA ‘KUTOBOA’

LAGOS, Nigeria WAHENGA walisema maisha ni safari yenye milima na mabonde. Kwamba katika kuishi kwako, si nyakati zote zitakuwa...

KIFO CHA BOSI KINAVYOITESA LEICESTER CITY

LONDON, UingerezaMIAKA 10 iliyopita, Leicester City waliishangaza dunia walipotwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya England (EPL) mbele ya...