DAR ES SALAAM
MWANDISHI na Mhariri mkongwe nchini, Revocatus Makaranga amefariki dunia leo Machi 5, 2026 muda mfupi baada ya kufikishwa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH).
Kwa mujibu wa taarifa za awali kutoka kwa ndugu wa karibu, Makaranga alikimbizwa Hospitali ya Taifa Muhimbili kwenye kitengo cha dharura kwa ajili ya kupatiwa matibabu.
Hata hivyo, licha ya jitihada za madaktari kumhudumia, alifariki muda mfupi baada ya kufikishwa hospitalini.
Marehemu Makaranga ni mmoja wa waandishi na wahariri wakongwe nchini waliotoa mchango mkubwa katika tasnia ya habari nchini Tanzania.
Makaranga mbali na kufanya kazi katika vyombo vya habari vya umma wakati wa mfumo wa chama kimoja na baadaye vyama vingi, pia alifanya kazi katika kampuni za binafsi za habari za Mwananchi Communications Ltd (MCL), New Habari Ltd.
Makaranga ni mhitimu wa shahada ya uzamili katika uandishi wa habari kutoka Chuo Kikuu cha Cardiff, Wales, Uingereza.
