TANZANIA, INDIA KUIMARISHA USHIRIKIANO

Date:

Share post:

ZERUBABEL CHUMA

SERIKALI za Tanzania na India zinakusudia kuimarisha ushirikiano katika sekta ya ulinzi.

Hayo yamesemwa juzi na Makamu wa Rais, Dkt. Philip Mpango alipokuwa akizungumza na Naibu Waziri wa Ulinzi wa India, Sanjay Seth, Ikulu Dar es Salaam

Dkt. Mpango alisema ziara aliyofanya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan nchini India, Oktoba 2023 imeimarisha zaidi uhusiano uliopo.

Alisema ushirikiano unaokusudiwa ni kubadilishana mafunzo ya kijeshi na viongozi wa Wizara za Ulinzi  wa Tanzania na India kutembeleana.

Alipongeza zoezi la pamoja la kijeshi la nchi hizo mbili na nchi washirika kutoka Afrika lililohusisha Jeshi la Wanamaji na maonesho ya zana na vifaa vya ulinzi.

Alitaja maeneo mengine ambayo Tanzania inashirikiana na India katika masuala ya ulinzi kuwa ni mafunzo ya pamoja ya kijeshi ya kudhibiti ugaidi, kupambana na uharamia, uokoaji na doria za pamoja.

Aidha, alipongeza ushirikiano uliopo kwa nchi hizo mbaili katika masuala ya afya, elimu, Maji, usafiri na huduma zingine za kijamii.

Nibu Waziri wa Ulinzi wa India, Sanjay Seth na ujumbe wake, alipokutana na kuzungumza na Makamu wa Rais, Dkt Philip Mpango, Ikulu, Dar es Salaam.

Kwa upande wake Naibu Waziri wa Ulinzi wa India, Sanjay Seth alisema Tanzania imeimarisha zaidi ushirikiano na India na hivi sasa ni mshirika wa kuaminika katika sekta mbalimbali za kiuchumi na kijamii ikiwemo biashara, uwekezaji, maji, afya na elimu.

Sanjay alisema Tanzania ni nchi ya pili barani Afrika kwa ufanyaji biashara na India ikitarajiwa kufikia Dola za Marekani, bilioni nane mwaka 2024/2025.

Mazungumzo hayo yalihudhuriwa na Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Balozi Dkt. Stergomena Tax, Balozi wa India nchini Tanzania, Bishwadip Dey pamoja na viongozi mbalimbali wa Jeshi la Ulinzi kutoka Tanzania na India.

About The Author

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

USIYOYAJUA KUHUSU KOCHA ALIYEANDIKA HISTORIA BUNDESLIGA

MUNICH, Ujerumani JINA la Marie-Louise Eta limeandika historia katika soka la Ujerumani baada ya kuwa mwanamke wa kwanza kuwa...

BURNA BOY HATAKI MAZOEA, ‘BIFU’ KWAKE KAWAIDA TU

HIVI karibuni, supastaa wa muziki wa Afrobeat, Burna Boy, aliingia kwenye mikono ya Chama cha 'Ma-dj' nchini Nigeria,...

BURKINA FASO IKO HOI AU HAI CHINI YA KAPTENI TRAORE?

HATUA ya kutangaza kuwa raia wake waaitarajie demokrasia imeibua maswali mengi juu ya uongozi wa Kapteni Ibrahim Traore...

SIMU YAKO CHANZO CHA UGONJWA WA MOYO, SARATANI?

UKWELI ulio wazi ni kwamba matumizi ya simu za mkononi yameongezeka kwa kasi duniani, Tanzania ikiwa na 'laini'...