TPDC, ZPDC KUSHIRIKIANA SEKTA YA GESI

Date:

Share post:

RIPOTA PANORAMA

NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga amesema Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) na Shirika la Maendeleo ya Petroli Zanzibar (ZPDC) yamesaini makubaliano ya kushirikiana katika mambo mbalimbali.

Akizungumza mapema wiki bungeni mjini Dodoma, Kapinga alisema makubaliano hayo yalisainiwa Februari, 2022 na hivi sasa, pamoja na mambo mengine TPDC na ZPDC zinashirikiana kwa kubadilishana ujuzi na utaalamu.

Akijibu swali la Mbunge wa Kwahani, Khamis Yussuf Mussa Mkenge aliyeuliza ni lini serikali itainufaisha Zanzibar katika matumizi ya Nishati ya Gesi ili iweze kutumika katika magari, alisema ajenda iliyopo sasa ni kupeleka gesi Zanzibar.

“Mheshimiwa Spika katika ushirikiano huu, suala la kupeleka gesi Zanzibar ni mojawapo ya ajenda kuu. Pande zote mbili bado zinaangalia namna bora ya kufikisha gesi asilia Zanzibar ili iweze kupatikana kwa bei nafuu kwa watumiaji,”. alisema Kapinga

About The Author

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

USIYOYAJUA KUHUSU KOCHA ALIYEANDIKA HISTORIA BUNDESLIGA

MUNICH, Ujerumani JINA la Marie-Louise Eta limeandika historia katika soka la Ujerumani baada ya kuwa mwanamke wa kwanza kuwa...

BURNA BOY HATAKI MAZOEA, ‘BIFU’ KWAKE KAWAIDA TU

HIVI karibuni, supastaa wa muziki wa Afrobeat, Burna Boy, aliingia kwenye mikono ya Chama cha 'Ma-dj' nchini Nigeria,...

BURKINA FASO IKO HOI AU HAI CHINI YA KAPTENI TRAORE?

HATUA ya kutangaza kuwa raia wake waaitarajie demokrasia imeibua maswali mengi juu ya uongozi wa Kapteni Ibrahim Traore...

SIMU YAKO CHANZO CHA UGONJWA WA MOYO, SARATANI?

UKWELI ulio wazi ni kwamba matumizi ya simu za mkononi yameongezeka kwa kasi duniani, Tanzania ikiwa na 'laini'...