DKT. BITEKO AINYOSHEA KIDOLE TANESCO

Date:

Share post:

TERESEA MHAGAMA

NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Dotto Biteko amemuagiza Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Ugavi wa Umeme (Tanesco), Mhandisi Gissima Nyamo – Hanga kumchukulia hatua mtumishi wa shirika hilo aliyemfokea mteja.

Amesema iwapo Mhandisi Nyamo – Hanga hatatekeleza agizo hilo, yeye mwenyewe atachukua hatua kwa mtumishi huyo.

Agizo hilo amelitoa hivi karibuni kwenye kikao cha tatu cha tathmini ya utendaji kazi wa taasisi zilizo chini ya Wizara ya Nishati kwa kipindi cha miezi mitatu, Oktoba hadi Disemba 2024.

Dkt. Biteko ameanzisha utaratibu wa kufanya vikao vya tathmini ya utendaji kazi wa taasisi zilizo chini ya wizara yake kwa lengo la kujipima na kuboresha utendaji kazi wa taasisi hizo.

Alisema haridhishwi na mwenendo wa kituo cha huduma kwa wateja cha Tanesco ambacho kinalalamikiwa na wateja.

“Pamoja na kazi nzuri mnazozifanya lakini eneo ambalo bado hatujafanya vizuri ni utoaji wa huduma kwa wateja. Juzi nilitembelea kituo hiki nikawaambia sifurahishwi na utendaji kazi wa kituo.

“Mimi nafahamu changamoto za kituo hiki si kwa kuota bali wananchi wananipa mrejesho pamoja na viongozi wanaonisimamia. Hivi tumefanya kazi yote
hii ya kuwa na umeme wa ziada, tunajenga laini za umeme lakini mtu mmoja ambaye kazi yake ni kumsikiliza mteja na kumpa majibu sahihi anatupainti wote vibaya tunaonekana hatufai.

“Majibu yapo lakini wataalamu wanageuka kuwa wababe kwa wateja, hii haikubaliki,” alisema Dkt. Biteko.

Alilitaja lalamiko la mwananchi aliyepiga simu Tanesco kisha akapewa tiketi namba ya lalamiko lakini baada ya muda ilifutwa kwa madai kwamba lalamiko husika limeshashughulikiwa wakati halijashughulikiwa.

Alisema mteja huyo alipouliza kwanini lalamiko lake lake limefutwa alifokewa na mtumishi wa Tanesco.

About The Author

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

USIYOYAJUA KUHUSU KOCHA ALIYEANDIKA HISTORIA BUNDESLIGA

MUNICH, Ujerumani JINA la Marie-Louise Eta limeandika historia katika soka la Ujerumani baada ya kuwa mwanamke wa kwanza kuwa...

BURNA BOY HATAKI MAZOEA, ‘BIFU’ KWAKE KAWAIDA TU

HIVI karibuni, supastaa wa muziki wa Afrobeat, Burna Boy, aliingia kwenye mikono ya Chama cha 'Ma-dj' nchini Nigeria,...

BURKINA FASO IKO HOI AU HAI CHINI YA KAPTENI TRAORE?

HATUA ya kutangaza kuwa raia wake waaitarajie demokrasia imeibua maswali mengi juu ya uongozi wa Kapteni Ibrahim Traore...

SIMU YAKO CHANZO CHA UGONJWA WA MOYO, SARATANI?

UKWELI ulio wazi ni kwamba matumizi ya simu za mkononi yameongezeka kwa kasi duniani, Tanzania ikiwa na 'laini'...