KIWANDA CHA BETRI GRAVITA CHAFUKIA KEMIKALI HATARI ARDHINI

Date:

Share post:

 


RIPOTA PANORAMA

0711 46 49 84

KIWANDA cha kutengeneza betri za magari cha Gravita kilichopo eneo la ukanda wa viwanda, Misugusugu, Wilaya ya Kibaha, Mkoa wa Pwani kimezika ardhini kemikali zenye madhara kwa afya ya udongo na binadamu.
Habari za kuaminika zilizofikia Tanzania PANORAMA Blog kutoka ndani ya kiwanda hicho zimeeleza kuwa kemikali zilizofukiwa ardhini ni zile zilizokwishatumika kutengenezea betri za magari ambazo zinapaswa kuteketezwa na si kuzikwa ardhini. 
 
Watoa taarifa wetu kutoka ndani ya kiwanda hicho wameeleza kuwa kazi ya kuzika ardhini kemikali hiyo hatari hufanyika siku za mwiahoni mwa wiki ambapo wafanyakazi wengi wanakuwa wamepumzika na waliongeza kuwa ni kazi inayofanyika wakati wa usiku tu.
 
Vyanzo zaidi vya habari vya Tanzania PANORAMA Blog kutoka ndani ya kiwanda hicho vimeeleza kuwa kina miubdombinu mizuri iliyopasishwa na Baraza la Taifa la Usimamizi wa Mazingira (NEMC) ya uteketezaji kemikali zinazotumika kwa shughuli za viwandani lakini haitumiki ipasavyo.
 
“Kuna mambo ya hatari sana yanafanyika hapa kiwandani. Hizi betri kuzitengeneza kuna kemikali hutumika na hiyo kemikali inapaswa kuteketezwa kabisa baada ya kutumika.  Hapa kiwandani kuna miundombinu mizuri tu ya uteketezaji wq kemikali hiyo lakini haitumiki ipasavyo kwa sababu hawa jamaa wanakwepa gharama.

“Badala yake wanatumia njia hii ya kufukua mashimo na kuzika hiyo kemikali. Hili eneo likija kuchungzwa litakutwa na kemikali ardhini na ujue madhara yske ni kwamba hii kemikali inasambaa huko ardhini, baada ya muda eneo lote hili litakuwa la ardhi iliyokufa kwa sababu ya kemikali wanayoizika hawa jamaa.

“^Wanachokifanya siku za mwsho wa wiki ambazo wafanyakazi wengi hawaji kazini wao humwambia dreva wa greda kuchimba mashimo ambayo kemikali hiyo huzikwa humo kisha greda hilo hufukia hayo mashimo.

“Vizazi vyetu vitakuja kuishi kwenye eneo lililokufa kwa sababu ya tamaa ya kupata pesa nyingi ya hawa jamaa. Ushahidi kamili upo na wewe tunakupa ili wakibisha tu muutoe. Na hata pakija kupimwa hapa wataalamu watagubdua kemikali nyingi tu inazikwa ardhini,” alisema mtoa taatifa wetu.

Tanzania PANORAMA Blog iliutafuta uongozi wa kiwanda hicho kwa njia ya simu kuzungumzia suala hilo. Katika majibu yake afisa aliyetambulika kwa jina la Goodluck Komba ambaye hata hivyo alikataa kueleza nafasi yake aliomba kukutana na Tanzania PANORAMA Blog ofisini kwake kwa mazungumzo na alipoambiwa lengo la kupigiwa simu siyo kuketi chini kwa mazungumzo bali kujibu maswali aliyoulizwa alilisitiza kuwa anahitaji mazungumzo.

Tanzania PANORAMA Blog itachapisha ripoti maalumu kuhusu kemikali hizo hatari zinavyofukiwa ardhini na kiwanda hicho na madhara yake kwa ardhi na watu wanayoitumia.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

SOMA HIYO! ISRAEL NDIYO WAASISI WA MIKWAJU YA PENALTI

LONDON, Uingereza NI jioni ya Agosti 5, 1970 kwenye Uwanja wa Boothferry Park mjini Hull, Manchester United ikiwa ugenini...

AMEJIPATA! LAMPARD ALIVYOREJEA EPL AKIWEKA REKODI

LONDON, Uingereza IKIWA ni miezi 18 tu imepita tangu alipoajiriwa, Frank Lampard ameiwezesha Coventry City kupanda daraja na kurejea...

USICHUKULIE POA! PATORANKING ALIUZA SUMU YA PANYA MITAANI KABLA YA ‘KUTOBOA’

LAGOS, Nigeria WAHENGA walisema maisha ni safari yenye milima na mabonde. Kwamba katika kuishi kwako, si nyakati zote zitakuwa...

KIFO CHA BOSI KINAVYOITESA LEICESTER CITY

LONDON, UingerezaMIAKA 10 iliyopita, Leicester City waliishangaza dunia walipotwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya England (EPL) mbele ya...