Date:

Share post:

Mwanamuziki Misri afungwa kwa kukashifu Mto Nile


Mwanamuziki maarufu wa Misri, Sherine Abdel Wahab amehukumiwa kifungo cha miezi sita gerezani kwa kukashifu usafi wa Mto Nile.
Sherine ambaye pia ni jaji katika kipindi cha mashindano ya waimbaji yanayojulikana kwa jina la The Voice alitiwa hatiani na mahakama wiki hii baada ya kushitakiwa kwa kosa la kuukashifu Mto Nile.
Ilidaiwa mahakamani kuwa mwanamuziki huyo, aliwaambia wapenzi wa mashabiki wake wakati wa onyesho lake nchini huko kwamba kunywa maji ya Mto Nile kunaweza kumpatia vijidudu.
Sherine alifunguliwa mashitaka mwezi Novemba mwaka jana baada ya video yake kusambazwa mtandaoni ikimuonyesha akiombwa kuimba wimbo uitwao Mashrebtesh Men Nilha (umewahi kunywa maji ya Mto Nile?).
Katika video hiyo, Sherine alionekana akiwajibu wapenzi na mashabiki wake kuwa ‘Nikinywa maji ya Mto Nile nitapata kichocho.’
Nchini Misri, ugonjwa wa kichocho unawapata zaidi wananchi wa vijijini.
Aidha, chama cha wanamuziki nchini Misri kimetangaza kuupiga marufuku marufuku wimbo huo kuibwa Misri.
Wakati huo huo, mwanamuziki mwingine, Laila Amer naye mapema wiki hii alihukumiwa kifungo cha miaka miwili gerezani baada ya kupatikana na hatia ya uchochezi, ufitini na uovu.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

KIFO CHA BOSI KINAVYOITESA LEICESTER CITY

LONDON, UingerezaMIAKA 10 iliyopita, Leicester City waliishangaza dunia walipotwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya England (EPL) mbele ya...

ISHU YA RASHFORD BADO PASUA KICHWA

MANCHESTER, UingerezaKOCHA wa Manchester United, Michael Carrick, amesema bado haijafahamika kama Marcus Rashford atarudi klabuni hapo au atabaki...

BARCA YAPATA MRITHI WA LEWANDOWSKI

CATALUNYA, HispaniaKLABU ya Barcelona imeanza mipango ya kumsajili mshambuliaji wa kati wa Real Mallorca, Vedat Muriqi, ikiamini anatosha...

ARSENAL AKILI YOTE KWA MONGA

LONDON, UingerezaARSENAL ya Kaskazini mwa Jiji la London imeonesha nia ya kumsajili winga anayefanya vizuri Ligi Daraja la...