Kwa mujibu ya taarifa iliyotolewa jana na Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipa Kodi, Richard Koyombo, lengo lililokusudiwa ni katika wiki hiyo ni kuelimisha, kusikiliza malalamiko, changamoto na kupokea mrejesho na maoni mbalimbali kutoka kwa walipakodi.
Alisema pamoja na masuala mengine, TRA itatumia wiki hiyo kutoa elimu ya ulipaji kodi ya majengo kwa njia ya kielektroniki, elimu kuhusu mkataba wa huduma kwa mlipa kodi na matumizi sahihi na umuhimu wa kutumia Mashine za Kielektroniki za Kutolea Risiti (EFDs).
Pia, itatoa elimu kwa wananchi kuhusu umuhimu wa kudai na kutoa risiti kila wanapouza au kununua bidhaa na huduma mbalimbali.
Aidha, utafanyika usajili wa walipakodi wapya kwa mwaka wa fedha wa 2017/18 mamlaka. TRA imekusudia kusajili walipakodi wapya 1,000,000 nchi nzima.
Wiki ya mlipa kodi kuanza Machi 5
Wiki ya mlipa kodi kuanza Machi 5
Wiki ya elimu kwa mlipa kodi inatarajiwa kuanza Machi 5 hadi 9 katika mikoa yote nchini.