KUFA KWA MAGAZETI YA KAMPUNI YA NHL KWAIBUA UPYA MACHUNGU YA WANAOIDAI

Date:

Share post:

 

Hussein Bashe

 NA MWANDISHI WETU

MATUMAINI ya waliokuwa wafanyakazi wa Kampuni ya New Habari (2006) Ltd na awali, Habari Corporation Ltd ya kulipwa pensheni zao baada ya kuondolewa kazini kinyuime cha utaratibu yamezidi kutoweka baada ya kutolewa tangazo na kusitishwa kwa uchapishaji wa magazeti yanayozalishwa na kampuni hiyo kwa sababu ya ukata.

Tangazo la kusitishwa kwa uchapishaji wa magazeti yaliyokuwa yakizalishwa na New Habari (2005) Ltd ya Mtanzania, Rai, Dimba na Bingwa lilitolewa jana katika mitandao ya kijamii ikimkariri Mhariri Mtendaji, Dennis Msacky kuwatangazi wafanyakazi wanaodaiwa kuidai kampuni mshahara wa zaidi ya miezi mitatu, uamuzi huo sambamba za kupunguza wafanyakazi.

Taarifa ya kusitishwa kwa uzalishaji wa magazeti hoyo ilisomeaka; “Kampuni ya New habari 2006 LTD inayozalisha magazeti ya Mtanzania, Rai, Bingwa, Dimba imetangaza kusitisha uzalishaji za magazeti yote kutokana na mwenendo mbaya wa kibiashara.

“Akizungumza na wafanyakazi wa kampuni hiyo, Mhariri Mtendaji, Dennis Msacky amesema uzalishaji wa magazeti hayo utasitishwa kuanzia jumatatu ijayo.” 

Muda mfupi baada ya kusambaa kwa taarifa hiyo, zaidi ya watu 150 waliokuwa wafanyakazi wa Kampuni New Habari waliopunguzwa bila kulipwa pensheni zao ingawa walikuwa wakikatwa kila  mwezi, walianza kuelezea hisia za kuibuliwa upya kwa machungu ya kupoteza haki zao kwa kueleza kuwa hawana tena uhakika wa kuzipa.

Afisa Mtendaji Mkuu wa New Habari, Erasto Matasia alipotafutwa kupitia simu yake ya kiganjani kuzungumzia suala hilo alisema yuko msibani na kwamba aliyeteuliwa na kampuni kuzungumzia usitishwaji huo na kupunguzwa wafanyakazi kwa niaba ya Hussein Bashe ni Msacky.

“Mimi sipo huko, niko msibani, nakushauri mtafute Dennis Msacky aliyeteuliwa na kampuni kulizungumzia jambo hilo kwa niaba ya Bashe,” alisema Matasia.

Jitihada za kumpata Msacky hazikuweza kuzaa matunda baada ya simu yake ya kiganjani kuwa anaizima kila alipopigiwa na kuita.

Kampuni ya New Habari na kabla ya hapo ikifahamika kwa jina la Habari Corporation inaandamwa na madeni makubwa ya miaka mingi ya waliokuwa wafanyakazi wake ambao walikuwa wakikatwa fedha kwa ajili ya pensheni zao lakini baadhi ya viongozi wa juu wa kampuni hiyo walikuwa wakizitia kibindoni.

Bashe, ambaye kabla ya kuchaguliwa kuwa mbunge alikuwa Afisa Mtendaji Mkuu wa New Habari 2006 LTD, amepata kukaririwa na baadhi ya vyombo vya habari akikiri kuchota fedha za kampuni hiyo na kuzitumia katika biashara zake binafsi na kwamba alikuwa na matarajio ya kuzirejesha baada ya kupata faida.

Tanzania PANORAMA Blog inaendelea na ufuatiliaji wa sakata hili

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

SOMA HIYO! ISRAEL NDIYO WAASISI WA MIKWAJU YA PENALTI

LONDON, Uingereza NI jioni ya Agosti 5, 1970 kwenye Uwanja wa Boothferry Park mjini Hull, Manchester United ikiwa ugenini...

AMEJIPATA! LAMPARD ALIVYOREJEA EPL AKIWEKA REKODI

LONDON, Uingereza IKIWA ni miezi 18 tu imepita tangu alipoajiriwa, Frank Lampard ameiwezesha Coventry City kupanda daraja na kurejea...

USICHUKULIE POA! PATORANKING ALIUZA SUMU YA PANYA MITAANI KABLA YA ‘KUTOBOA’

LAGOS, Nigeria WAHENGA walisema maisha ni safari yenye milima na mabonde. Kwamba katika kuishi kwako, si nyakati zote zitakuwa...

KIFO CHA BOSI KINAVYOITESA LEICESTER CITY

LONDON, UingerezaMIAKA 10 iliyopita, Leicester City waliishangaza dunia walipotwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya England (EPL) mbele ya...