MLIPUKO KIWANDA CHA FATAKI WAUA WATU 21 CHINA

Date:

Share post:

BEIJING, China

MLIPUKO uliotokea katika kiwanda cha utengenezaji wa fataki umesababisha vifo vya watu 21 na kujeruhi wengine 61.

Kwa mujibu wa taarifa, tukio hilo limetokea jana Mei 4, 2026 katika Jimbo la Hunan mjini Liuyang.

Mamlaka za Liuyang zilitumia wataalamu wa uokoaji takribani 500 kuendesha zoezi la kutafuta walionasa kwenye jengo la kiwanda hicho.

Kwa upande mwingine, majeruhi wa mlipuko huo wametajwa kuwa na umri wa kuanzia miaka 20 hadi 60.

Taarifa zaidi zinaeleza kuwa polisi wanaendelea na uchunguzi ili kubaini chanzo cha mlipuko huo.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

BAHI YA TUMIA MICHEZO KUHAMASISHA MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

Wilaya ya Bahi mkoani Dodoma imezindua kampeni maalum ya kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia kupitia mashindano...

RC MAKALLA ARIDHISHWA NA MAENDELEO YA UJENZI WA UWANJA NA BARABARA ZA AFCON ARUSHA

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Amos Gabriel Makalla amesema ameridhishwa na maendeleo ya ujenzi wa uwanja wa michezo...

RUTO ATAJA UWEKEZAJI WA KENYA TANZANIA KUFIKIA DOLA BILIONI 1.7, AONYA URASIMU MIPAKANI

Rais wa William Ruto amesema kuwa takribani kampuni 500 kutoka Kenya zimewekeza jumla ya dola za Marekani bilioni...

RUTO ASISITIZA USHIRIKIANO WA EAC NI UFUNGUO WA KUKUZA BIASHARA NA AJIRA KWA WANANCHI

Rais wa William Ruto amesema nchi za Afrika Mashariki zina fursa kubwa ya kuongeza biashara ya ndani na...