WASHINGTON DC, Marekani
RAIS Donald Trump amesema Marekani imezishambulia boti mbili za Iran katika Mlango-Bahari wa Hormuz.
Mkondo-Bahari huo wa Hormuz umekuwa sehemu muhimu ya mgogoro kati ya Iran na mahasimu wake, Marekani na Israel.
Hormuz ndiyo njia inayotumiwa kwa usafirishaji wa asilimia 20 ya rasilimali za mafuta na gesi duniani.
Aidha, hatua ya Marekani kuzishambulia boti hizo inakuja wakati Taifa hilo likiwa limeshatangaza kudhibiti meli zote zitakazokatika eneo hilo.
Wakati huo huo, jana Mei 4, 2026, Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) na Korea Kusini nazo ziliripoti meli zake kushambuliwa.






